• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Nataka kila mtumishi apande miti 10 – RC Mahenge

Imewekwa tarehe: January 9th, 2021

WATUMISHI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kupanda miti 10 kila wiki ikiwa ni utekelezaji wa kampeni ya kukijanisha Dodoma na kulifanya Jiji la Dodoma kuwa na hali nzuri ya hewa na mazingira.

Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge baada ya kuongoza zoezi la upandaji miti katika eneo la Medeli jijini humo leo.

Dkt. Mahenge aliagiza kuwa, kila mtumishi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma apande miti 10 kwa wiki. “Nataka kila mtumishi kuanzia leo, kila wiki lazima apande miti 10. Miti hiyo nataka iwekewe alama au jina lake ili iwe rahisi kutambulika” alisema Dkt. Mahenge. 

Katika kulifanya zoezi hilo kuwa na umuhimu alishauri kuwa watumishi wanaweza kushirikisha familia au marafiki zao katika kupanda miti hiyo na kwamba utekelezaji wa zoezi hilo utakaguliwa na kuingizwa katika taratibu za kiutumishi ili iwe rahisi kuchukua hatua stahiki kwa mtumishi atakayeshindwa kutekeleza.

Mkuu huyo wa Mkoa alikemea tabia ya baadhi ya watu kudharau zoezi la upandaji miti na utunzaji wa mazingira jijini hapa. “Kuna baadhi ya watu wanadhani mabadiliko ya kuifanya Dodoma ibadilike na kuwa ya kijani ni la watu wengine. Dhana hiyo siyo sahihi, jukumu hili ni letu sote, watu wanasubiri mazingira yatengenezwe na kuwa mazuri kisha waje kufanyia sherehe. Upandaji miti na utunzaji mazingira ni wajibu siyo ‘ceremonial" alisema Mkuu huyo wa Mkoa.

Akisoma taarifa fupi ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mkuu wa Idara ya Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu, Dickson Kimaro alisema kuwa, katika kufanikisha kampeni ya kijanisha Dodoma ifanikiwe ni jukumu la kila mwana Dodoma na wadau kupanda miti kwenye maeneo mbalimbali kwa lengo la kuboresha Mazingira ya Dodoma.

“Halmashauri ya Jiji la Dodoma imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali za kuhakikisha lengo ya kuifanya Dodoma kuwa ya kijani linafanikiwa. Jitihada hizo ni pamoja na utengaji na uainishaji wa maeneo mahsusi kwa ajili ya kupanda miti, uendelezaji wa bustani za kuzalisha miche, utoaji wa elimu kwa umma kuhusu Dodoma ya kijani pamoja na kuweka Mazingira wezeshi kwa wadau mbalimbali wenye nia ya kuunga mkono na kuendeleza jitihada za Serikali za kuifanya Dodoma kuwa ya kijani” alisema Kimaro.

Akiongelea mikakati ya Halmashauri katika kukijanisha Dodoma, aliitaja kuwa ni kuhakikisha kila mwananchi anashiriki katika upandaji miti ambapo kila mkazi wa Dodoma anatakiwa kupanda miti angalau mitano katika eneo lake ikienda sambamba na kudhibiti ukataji miti ovyo bila ya kibali cha Afisa Mwidhinishaji kutoka Jiji.

Mikakati mingine aliitaja kuwa ni “Sheria ndogo za utunzaji na usimamizi wa Mazingira za Jiji la Dodoma zimesambazwa katika Kata na Mitaa ili kudhibiti mifugo inayokula miti iliyopandwa na uvamizi wa jamii kwenye misitu ya asili. Pia kutoa elimu ya upandaji miti kulingana na majira ya mvua katika Kata 41 za Halmashauri ya Jiji na kuhamasisha upandaji miti kuanzia kwenye ngazi ya kaya, taasisi na uanzishwaji wa mashamba ya miti kwa mitaa yenye maeneo makubwa kwa njia ya matangazo ya barabarani” alisema Kimaro.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru alisema Halmashauri hiyo yenye ukubwa wa kilometa za mraba 2,576 itaendelea kushirikisha wadau mbalimbali katika utekelezaji wa kampeni ya kijanisha Dodoma huku akimshukuru Mkuu wa Mkoa huo, Mkuu wa Wilaya, na wadau wote waliojitokeza kwa wingi katika utekelezaji wa zoezi hilo.

Katika zoezi hilo la upandaji miti lililoongozwa na Mkuu wa Mkoa, lilihudhuriwa na wakuu wa taasisi mbalimbali, wanafunzi kutoka vyuo vikuu na wananchi,  jumla ya miti 2,140 ilipandwa.

Kampenzi ya kijanisha Dodoma ilizinduliwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan Disemba 21, 2017 kwa kupanda miti katika bonde la chanzo cha maji cha Mzakwe Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru akipanda mti katika zoezi lililoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Binilith Mahenge

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Biilith Mahenge (wa kwanza kulia) akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma alipokuwa akielezea kuhusu utekelezaji wa zoezi la kupanda miti Jijini Dodoma pamoja na mikakati kuhakikisha kuwa zoezi la upandaji miti linakukwa endelevu.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.