• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Nchi ipo salama, tutaendelea mbele – Rais Mhe. Samia Hassan

Imewekwa tarehe: March 22nd, 2021

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan amesema kuwa nchi ipo salama na ataendeleza yale ambayo aliyekuwa Rais, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli alitamani kuyafikisha kwa maslahi ya watanzania.

Rais, Mama Hassan amesema hayo leo alipokuwa akitoa salamu katika uwanja wa Jamhuri jijini hapa katika zoezi la kitaifa la kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati Dkt. John Mafuguli.

Rais, Mama Hassan amesema “Nchi yetu ipo katika mikono salama, mimi na mwenzangu Rais, wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Mwinyi tutaendeleza na tutafika pale alipotamani Hayati Dkt. John Pombe Magufuli”.

“Katika uongozi wake tumejifunza vizuri, tumepikwa vizuri na tumeiva sawasawa. Tupo tayari kuendeleza kazi yake nzuri kwa nguvu, kasi na ari ile ile. Kwa wale ambao wanamashaka, mwanamke huyu ataweza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nataka niwaambie kwamba aliyesimama hapa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye maumbile yake ni mwanamke” amesema Rais huyo kwa kujiamini.

Akiongelea mahusiano ya Tanzania na nchi jirani, Rais huyo amesema uwa mahusiano hayo yataendelea kuwa imara na kuimarika zaidi chini ya uongozi wake.

Akimuongelea mwenda zake Hayati Dkt. Magufuli, amesema kuwa katika kipindi cha miaka sita ya utawala wake alijenga uchumi wa ndani unaotegemea mapato ya ndani, akiwekeza katika ujenzi wa miradi ya kimkakati. “Rais, Dkt. Magufuli alidhamiria kufungamanisha ukuaji wa uchumi na maendeleo ya watu kwa kuboresha upatikanaji wa huduma za kijamii kama afya na elimu. Kutokana na dhamira hiyo, leo watanzania wengi wanyonge na masikini wanamlilia” amesema Rais Mama Hassan.

Hofu yake kwa Mungu ndiyo iliyomfanya kuwa na mapenzi makubwa kwa wanyonge na masikini wa Tanzania, hakuwahi kukosa muda wa kusali na kuabudu, aliongeza na kuwataka watanzania kutumia kipindi hicho cha maombolezo kumshukuru Mungu.

Rais Mama Hassan amesema kuwa Hayati Dkt. Magufuli hakuogopa kutetea alichoamini kuwa ni sahihi kwa maslahi ya Taifa hata kama kinahatarisha maisha yake. “Umati huu uliojitokeza na simanzi kubwa ni kielelezo tosha cha pigo kwa watanzania” amesema Rais, Mama Hassan.

Akiongelea imani ya Hayati Dkt. Magufuli kwake, amesema kuwa daima atamshukuru kwa imani kubwa aliyoiweka kwake na kwa wanawake wote wa Tanzania. “Tukiandika historia ya usawa, jina lake litakuwepo, kupitia yeye Tanzania ilipata nafasi ya mwanamke wa kwanza Makamu wa Rais na sasa Rais. Hii inanipa faraja kwa miaka sita nilihudumu kama msaidizi wake wa kwanza na wa karibu” amesema Rais, Mama Hassan.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, ambae pia ni Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi amesema kifo cha Hayati Dkt. Magufuli kimetingisha bara zima la Afrika. “Msiba huu siyo tu, unawagusa watanzania peke yao, kuondoka kwa Dkt. Magufuli kumetingisha bara zima la Afrika. Bara la Afrika linajikuta katika taharuki ya kupoteza mwanasiasa aliyekuwa anaboresha maisha ya wananchi wake na aliyelenga kutetea na kuboresha uchumi wa kijamii katika bara la Afrika” amesema Rais, Tshisekedi.

Mwenyekiti huyo wa Umoja wa Afrika, amesema kuwa watabaki na kumbukumbu ya Hayati Dkt. Magufuli kama mpiganaji, mzalendo, siyo tu kwa maslahi mapana ya Tanzania bali kwa Umoja wa Afrika.

Zoezi la kitaifa la kuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Tanzania limefanyika Kitaifa katika uwanja wa Jamhuri na kuhudhuriwa na viongozi wakuu wa Nchi tisa na viongozi wengine wa mashirika ya kimataifa na Mabalozi mbalimbali.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.