• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Ndege kubwa kuanza kutua Uwanja wa Dodoma Oktoba mosi

Imewekwa tarehe: September 14th, 2020

NDEGE kubwa aina ya Airbus (200-300) zinazobeba abiria hadi 132 zitaanza kutua rasmi katika Kiwanja wa Ndege Dodoma Oktoba Mosi mwaka huu baada ya ujenzi na urefushaji wa barabara za kurukia ndege kukamilika.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mhandisi wa Tanroads Mkoa wa Dodoma, Salome Kaganda wakati akitoa taarifa fupi kwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge aliyetembelea uwanja huo jana. Awali uwanjani hapo zilikuwa zikitua ndege za ukubwa wa kati kama Bombardier Dash 8 Q400 zikitoa huduma kwa abiria 76-78, sasa zitaanza kutua ndege kubwa hadi aina ya Airbus.

Akizungumza uwanjani hapo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge alisema hayo ni mabadiliko makubwa yaliyofanyika tangu Serikali ya Rais John Magufuli kuhamia jijini Dodoma.

Dkt. Mahenge alisema ujenzi na ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Dodoma umetumia zaidi ya Sh. Bilioni 25 na utakabidhiwa rasmi kwa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) Oktoba Mosi mwaka huu na ndege kubwa zitaanza kutua rasmi.

Akitoa maelezo, Mhandisi Kaganda alisema, ujenzi na urefushaji wa uwanja huo utakamilika katika kipindi cha wiki mbili zilizobaki kama mkataba unavyoonesha. Ujenzi huo ulianza Juni 2016, na ulihusisha ujenzi wa barabara ya kurukia ndege yenye urefu wa mita 2,500 na upana mita 30, barabara za viungio, maeneo ya kuegesha ndege na taa za kuongozea ndege nyakati za usiku.

“Mradi wa ujenzi huo unatekelezwa na kampuni ya M/S China Henan International Cooperation Limited (Chico) kwa gharama ya Sh. Bilioni 11 kwa miezi sita na kusimamiwa na wahandisi wa Tanroads na Taa),” alisema.

Ujenzi au urefushaji unaoendelea sasa unahusisha urefushaji wa barabara ya kurukia ndege kwa mita 250 na upana mita 30 eneo la kugeuzia ndege, eneo la kuegeshea ndege lenye urefu wa mita 80 na upana meta 70 na urefushaji uzio wa usalama kwa gharama ya Sh bilioni 3.5.

Pia ujenzi na ukarabati huo ulioanza Juni 2016 ulihuisha ulipaji fidia Sh bilioni 11.4 kwa wananchi 168 ambao waliathirika na upanuzi na urefushaji wa uwanja huo mita 550 na upana mita 150.

Hivyo urefushaji wa barabara za kurukia ndege kutoka mita 2,500 za sasa hadi mita 2,750 utawezesha ndege kubwa zenye uwezo wa kubeba abiria hadi 132 (airbus 220-300) kutua katika Kiwanja cha ndege cha Dodoma na hivyo kurahisisha huduma za usafiri katika Jiji la makao makuu ya nchi.

Akizungumza Meneja wa Uwanja wa Ndege (TAA) Dodoma, Bertha Bankwa alisema kutokana na ukarabati huo, uwanja huo utakuwa na uwezo wa kutua ndege kubwa, alisema awali uwanja huo zilikuwa zikitua ndege ndogo lakini ukarabati ukikamilika basi zitakuwa zikitua ndege kubwa usiku na mchana kazi yote imefikia asilimia 70.

Bankwa aliongeza kuwa, pamoja na kukamilika uwanja huo, bado kutakuwa na changamoto chache zikiwemo za majengo marefu karibu na uwanja pamoja na nyumba nne zilizo karibu na eneo la kugeuzia ndege mambo ambayo yanatafutiwa ufumbuzi chini ya uongozi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCCA) pamoja na taasisi mwambata jijini kuzungumzia changamoto hizo.

Taasisi zitakazokutana hivi karibuni kutafuta suluhisho kuhusu kuongeza eneo la kugeuzia ndege pamoja na majengo marefu karibu na uwanja ni pamoja na TAA, Wakala wa Barabara Mjini (Tanroads), Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) na taasisi nyingine.

Mkuu wa Mkoa Dkt. Mahenge alisema, atawasiliana na taaasisi hizo zinazokutana ili kuhakikisha zinatatua changamoto hizo ili ikifika Oktoba mosi ndege kubwa zianze kutua.

Meneja wa Uwanja wa Ndege (TAA) Dodoma, Bertha Bankwa akitoa maelezo kuhusiana na ujenzi wa kiwanja wa ndege Jijini Dodoma na faida za ujenzi huo baada ya kukamilika.


Moja ya maeneo ambayo yameongeza ukubwa na urefu wa Kiwanja cha Ndege cha Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.