• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

NHC kushirikisha wabia wenye Uwezo

Imewekwa tarehe: November 16th, 2022

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amelitaka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuhakikisha kuwa linachambua na kupitia kwa umakini wawekezaji watakaoleta maombi ya ujenzi wa miradi ya ubia na Shirika hilo ili kupata wawekezaji wenye uwezo wa kukamilisha ujenzi kwa viwango na wakati.

Amesema kuwa kupitia sera mpya ya ubia Serikali inatarajia kuona wawekezaji na shirika wanajenga ubia imara utakaosaidia ukuaji wa Sekta ya nyumba nchini ambayo ni muhimu katika kuchochea ukuaji wa uchumi.

Ameyasema hayo leo (Jumatano, Novemba 16, 2022) wakati akizindua sera ya ubia ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC). Lengo la sera hiyo ni kuishirikisha sekta binafsi kuwekeza mitaji yake katika kujenga nyumba na majengo makubwa yenye tija kwa uchumi wa Taifa.

Amesema kuwa ushirikishwaji wa sekta binafsi katika mbalimbali utaongeza kasi na kuwa chachu ya mabadiliko katika miji yetu, hivyo Serikali itashirikiana na wawekezaji kuondoa changamoto zitakazojitokeza ili azma ya kuwekeza mitaji katika sekta hiyo iweze kutimia.

Waziri Mkuu amesema amefurahi kuona kuwa Shirika hilo limedhamiria kuishirikisha sekta binafsi katika kujenga nyumba za ghorofa katika maeneo inayoyamiliki ambayo ama yamepitwa na wakati ama yana viwanja ambavyo havijaendelezwa.

“Huu ni uamuzi mzuri, unathibitisha kwa vitendo na kuunga mkono maono na maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuvutia wawekezaji kutoka sekta binafsi kuwekeza mitaji yao ili kukuza uchumi wa nchi yetu. Serikali inafahamu kuwa ushirikishwaji wa sekta binafsi utaongeza kasi ya ujenzi na kuwa chachu ya mabadiliko katika miji yetu.”

Waziri Mkuu Amesema kuwa tangu kuanza kwa sera ya ubia mwaka 2012 shirika hilo limeingia mikataba 194 na sekta binafsi ambapo mikataba 73 ilifutwa kwa sababu ya ukiukwaji wa masharti, mikataba 111 yenye thamani ya shilingi bilioni 300, utekelezaji wake umefanyika ambapo mikataba 81 yenye thamani ya shilingi bilioni 240 utekelezaji wake umekamilika na mikataba 30 yenye thamani ya shilingi bilioni 60 utekelezaji unaendelea.

Amesema takwimu zinaonesha kuwa Tanzania ina uhaba wa nyumba milioni tatu na mahitaji hayo yanaongezeka kwa wastani wa nyumba 200,000 kila mwaka. “Upungufu huo, unachangia wamiliki wa nyumba binafsi kutoza kodi kubwa na wakati mwingine kudai kodi ya mwaka mzima kwa mkupuo mmoja.”

Majaliwa amesema lengo la Serikali ni kuwezesha wananchi wengi zaidi kumiliki nyumba zinazojengwa na Shirika hilo na waendelezaji wengine wa nyumba, hivyo uamuzi huo wa kuishirikisha sekta bianfsi unaenda kuongeza idadi ya nyumba nchini na kupunguza pengo la uhaba wa nyumba.

Naye, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angelina Mabula amesema kuwa maboresho ya sera ya ubia ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) yamelenga kuongeza ufanisi na tija kwa wabia wa Shirika hilo.

Aliongeza kuwa Shirika hilo litafanya uchambuzi wa kina ili kupata wawekezaji makini ambao watashikiriki kikamilifu katika miradi mbalimbali na kuhakikisha wanaopata fursa hiyo ni wale wenye uwezo wa kuridhisha wa kukamilisha miradi kwa wakati na viwango.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa NHC Nehemia Mchechu amesema kuwa sera hiyo imezingatia fursa za uchumi katika kipindi hiki, mafanikio na changamoto katika sera zilizopita.

“Sera hii pia itaongeza uwazi na mtu akitaka kuwezekeza kwenye miradi yetu isiwe lazima kumfahamu mtu yeyote ili uweze kupata fursa za miradi ya Shirika la Nyumba”

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.