• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

NIT yahamasisha wanafunzi wa kike kusoma sayansi

Imewekwa tarehe: May 12th, 2021

JAMII imeshauriwa kuwahamasisha wanafunzi wa kike kuchangamkia masomo ya sayansi hasa fani za uhandisi wa Ndege ili watoe mchango katika Taifa lao.

Kauli hiyo ilitolewa na Mhandisi Matengenezo ya Ndege kutoka Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Mhandisi Castory Njako alipokuwa akiongea na walimu na wanafunzi waliotembelea banda wa chuo hicho katika maonesho ya kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu yanayoendelea katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Asilimia kubwa ya wanafunzi wanaokuja kujifunza katika fani za uhandisi wa Ndege ni wanaume. “Tunahitaji sana watoto wa kike kuhamasishwa ili wawe na ndoto za uhandisi wa matengenezo ya Ndege. Hamasa hii ifanyike kwa kuwajengea desturi ya wanafunzi kutembelea vyuo na maonesho kama haya kunawajengea hamasa ya kupenda masomo ya sayansi” alisema Mhandisi Njako.

Akizungumzia dhana ya ugumu wa masomo ya sayansi, alisema kuwa dhana hiyo inajengwa kuleta hofu. “Siyo masomo hayo ni magumu, ugumu ni uelewa wanafunzi wanaojengewa na jamii. Kimsingi kila somo ni gumu, hakuna masomo ambayo ni mepesi. Fani ya uhandisi wa Ndege msingi wake ni hesabu, fizikia, kemia na kiingereza” aliongeza Mhandisi huyo.

Kwa upande wake Afisa Uhusiano wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Ngusekela Daudi alisema kuwa chuo hicho kinatoa ulimu katika fani mbalimbali. Alizitaja fani hizo kuwa ni uhandisi wa Ndege, mitambo, mabomba ya mafuta na matengenezo ya Meli. Nyingine ni usimamizi wa usafirishaji, ualimu ubobezi teknolojia na hesabu, ukutubi na mawasiliano. Aidha, alitoa wito kwa elimu bora watembelee chuo hicho.

Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia inaendesha Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) kila mwaka kwa madhumuni ya kutambua, kuadhimisha, kujenga, kukuza na kuendeleza ubunifu wa watanzania katika nyanja za sayansi na teknolojia ili kuchangia juhudi za kuifanya Tanzania kuwa na uchumi wa kati unaoendeshwa na viwanja.

Matangazo

  • TANGAZO LA MABADILIKO YA TAREHE YA USAHILI October 03, 2025
  • TANGAZO LA MAJINA YA WASIMAMIZI JIMBO LA MTUMBA October 03, 2025
  • MAJINA YA WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA- DODOMA MJINI October 03, 2025
  • TANGAZO LA MAJINA YA MAKARANI WAOGOZAJI WAPIGA KURA October 03, 2025
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Rc Senyamule awasihi wawekezaji sekta binafsi kuwekeza Dodoma

    October 03, 2025
  • CCTV kamera mwarobaini wa wavunjifu wa sheria jiji la Dodoma

    October 02, 2025
  • Wadau wa afya wapongezwa kwa juhudi zakudhibiti vifo vya wajawazito

    October 01, 2025
  • UONGOZI WA KLABU YA MICHEZO OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA WAKUTANA NA RAS KAZUNGU

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.