• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Nitawatetea madaktari wanaotimiza wajibu wao - Waziri Jafo

Imewekwa tarehe: August 21st, 2019

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Seleman Jafo amesema kuwa atawatetea madaktari ambao watatimiza majukumu yao, lakini hatasita kuwachukulia hatua wale ambao wataenda kinyumbe na taratibu.

Waziri Jafo ameyasema hayo wakati akifungua kikao kazi cha Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kilichofanyika jana katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Convention Centre Jijini Dodoma.

Mhe. Jafo amesema kuwa madaktari wamekuwa wakijitoa kwa weledi mkubwa katika kuwahudumia wananchi ili kuhakikisha kuwa wanatoa huduma bora kwa jamii na kuleta mabadiliko katika sekta ya afya nchini.

“kuna watu wanafanyakazi usiku na mchana  tusipowalinda watu wanaofanyakazi  tutawaumiza,  siamini kama kweli mtumishi mmoja pekee anaweza kula fedha bila kuwa na ushirikiano na watu wengine, si kweli hata kidogo, tutende haki kwa watumishi wanaotoa huduma za afya nchini” Amesisitiza Mhe. Jafo

Amesema Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya wanaofanya vibaya wanapaswa kuadhibiwa lakini lazima haki itendeke katika kuwachukulia hatua ili kuleta usawa na kupunguza malalamiko kwa wataalam wa afya nchini.

Amewaagiza viongozi wa Halmashauri kutenda haki wakati wa kuwachukulia hatua watumishi kwa kufuata sheria na taratibu za utumishi wa umma na kuhakikisha wanafanya uchunguzi wa kina wa tuhuma zilizotolewa dhidi yao ili kujiridhisha ndipo watoe maamuzi  yaliyosahihi.

Mhe. Jafo amefafanua kuwa kumekuwepo na tabia ya baadhi ya viongozi kuwashusha madaraka Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya  bila kufuata sheria na taratibu za kiutumishi kwa kusikiliza majungu na uongo usiofanyiwa kazi jambo hili si haki, hivyo serikali itaendelea kuwatetea na kuhakikisha wanarudishwa kwenye nafasi zao.

Naye,  Naibu Katibu Mkuu  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhandisi Joseph Nyamhanga amesema kuwa Serikali imejenga miundombinu ya  huduma za afya ambapo  mpaka sasa vituo 470  vimekarabatiwa na kujengwa nchini  kwa gharama ya shilingi  bilioni 321.

Mhandisi Nyamhanga amewaagiza Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha wanasimamia utoaji wa huduma bora za afya kwa watumishi ili waweze kufanyakazi kwa bidi na kuhakikisha huduma za afya zinaboreka nchini.

Wakati huohuo Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo na Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Faustine Ndungulile amewataka Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha wanaweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha watumishi walio chini yao wanatoa huduma bora kwa jamii ili kuwavutia kupata huduma  hiyo kwenye vituo vya kutolea huduma ya afya vilivyojengwa nchini.

Pia, aliwataka kuweka mikakati ya kuimarisha hali ya lishe katika ngazi ya jamii ili kupunguza hali ya udumavu kwa wananchi.

Aidha Katibu Mkuu wa Afya, Maendeleo na Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Zainabu Chaula amewataka  Waganga hao wa Mikoa na Wilaya  nchini kuhakikisha wanafanyakazi kama timu kwa kudumisha umoja na ushirikiano ili kuhakikisha huduma zinazotolewa kwa jamii zinakuwa bora nchini.

Chanzo: Tovuti ya tamisemi (www.tamisemi.go.tz)


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.