• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Nzuguni waondolewa hofu kubomolewa Makazi

Imewekwa tarehe: June 12th, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imewaondolea hofu wananchi wa Kata ya Nzuguni ya kubomolewa makazi yao kutokana na ujenzi usiozingatia taratibu za Mipango Miji baada ya kukamilisha zoezi la upimaji shirikishi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la hilo Godwin Kunambi alipokuwa akiongea na wananchi wa Kata hiyo iliyopo Jijini hapa jana baada ya kukamilika kwa zoezi la upimaji shirikishi eneo la Nzuguni ‘A’.

Kunambi alisema “kwanza napenda kuwapongeza wataalam wangu kwa kazi nzuri mliyoifanya ya upimaji shirikishi katika eneo za Nzuguni A, kupitia zoezi hilo la upimaji shirikishi, hofu kwa wananchi imeondolewa, kwamba kesho watabomolewa makazi yao”.

Kunambi alisema zoezi hilo limetekelezwa na Halmashauri kwa lengo la kuwahakikishia wananchi makazi bora na salama kwa mujibu wa taratibu za Mipango Miji.

Akiongelea umuhimu wa zoezi hilo, Kunambi alisema kuwa kukamilika kwa zoezi la upimaji shirikishi kutawawezesha wananchi kupata hati halali za umiliki wa viwanja ambazo zitawawezesha kupata mikopo katika taasisi mbalimbali za kifedha na kwamba Halmashauri ya Jiji inadhamira ya kuona wananchi wake wanaishi katika makazi bora na kuwa na uwezo wa kifedha kupitia rasilimali zao ikiwemo ardhi.

Akiongelea migogoro ya mipaka kwa baadhi ya wananchi, Mkurugenzi huyo aliwahakikishia wananchi hao kuwa timu ya wataalam  wa kutosha kutoka Halmashauri wataweka kambi katika Kata ya Nzuguni ili kuhakikisha wananchi wote wenye changamoto wanahudumiwa na kugawiwa viwanja kwa mujibu wa taratibu.

Naye msimamizi wa mradi wa upimaji shirikishi Nzuguni A, Aisha Masanja alisema kuwa mradi huo utahudumia wananchi 5,942 ukiwa na jumla ya viwanja 11,160 vya matumizi mbalimbali.

Akiongelea faida za mradi huo, Masanja alisema kuwa mradi huo utawawezesha wananchi kujenga katika viwanja vilivyopimwa na kuwawezesha kupata hati za umiliki wa viwanja hivyo.

“Halmashauri ya Jiji itafungua barabara zote katika eneo la mradi wa Nzuguni A na kujenga huduma za kijamii kama shule, vituo vya afya na viwanja vya michezo” alisema Masanja.

Alizitaja faida nyingine kuwa ni kupanga Mji kwani Halmashauri itakabiliwa na tatizo la makazi holela iwapo mji utaachwa bila kupangwa na kusisitiza upimaji huo unaondoa tatizo la makazi holela na vilevile, upimaji huo utatatua tatizo la migogoro ya mipaka inayolalamikiwa na wananchi.

Baadhi ya wakazi wa Nzuguni A akiwemo Wilfred Chimosa wamepongeza juhudi za Serikali za kufanya upimaji shirikishi katika eneo hilo.

“Shukrani kwa taarifa iliyowasilishwa na Afisa wa Halmashauri kwani inaonesha kazi nzuri iliyofanywa na Halmashauri ya Jiji…Moyo wangu sasa umesuuzika na nawashukuru sana Halmashauri ya Jiji kwa kazi nzuri” alisema Chimosa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Mipango Miji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, David Bochela aliwataka wananchi wa Kata ya Nzuguni kusimamia maamuzi halali yaliyoamuliwa kuhusiana na mradi huo.

“Simamieni mlichoamua, nashauri mapungufu ya watu wachache wenye migogoro ya ardhi yatatuliwe kwa utaratibu uliowekwa, na waale ambao haturidhiki tusicheleweshe wengine kwa maslahi yetu” alisema Bochela ambaye ni Diwani wa Kata ya Mkonze Jijini humo.

Aidha, aliwataka wananchi hao kujikita kwenye shughuli za maendeleo kuliko kuzalisha migogoro isiyo na tija.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.