• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Ofisi ya Rais Ikulu haishikiki kuvuta Kamba

Imewekwa tarehe: January 28th, 2025

Na. Aisha Ibrahim, DODOMA

Timu ya Ofisi ya Rais Ikulu kuvuta Kamba (wanaume) imeibuka na ushindi wa alama 2-0 dhidi ya Timu ya Ofisi ya Rais Jiji Dodoma kuvuta Kamba (wanaume) katika upande wa wanawake Timu ya Ofisi ya Rais Ikulu ikiibuka na ushindi wa alama 2-0 dhidi Timu ya Ofisi ya Rais Jiji Dodoma katika mchezo huo.

Mchezo huo ulifanyika ndani ya Uwanja wa Jamhuri katika Bonanza la Watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma lililohusisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa pete, michezo ya jadi na tamasha la sanaa.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Michezo, Utamaduni na Sanaa Jiji la Dodoma, Patrick Moshi, aliwataka washiriki wa michezo mbalimbali kujiamini zaidi wawapo uwanjani ikiwa ni njia kufanikiwa na kupata ushindi katika michezo yao. “Siri ni kufanya mazoezi mapema na wakati wa mchezo ni kujiamini zaidi na hiyo ndio siri ya mafanikio” alisemaMoshi.

Mwamuzi wa mchezo wa kuvuta kamba, Idrisa Shabani aliwaomba washiriki wa michezo mbalimbali kuwa na tabia ya kufanya mazoezi mara kwa mara ili kuwajengea uwezo wa kukabiriana ipasavyo pindi wanapokuwa kwenye michuano na timu pinzani. “Watu waje kufanya mazoezi, kama tunavyoona Timu ya Ofisi ya Rais Ikulu ilikuwa imejipanga kwa kufanya mazoezi lakini Timu ya Ofisi ya Rais Jiji Dodoma ilikuwa haijajipanga na ndio maana wamefungwa” alisema Shabani.

Akizungumzia kuhusu mchezo huo wa kuvuta kamba, mmoja kati ya washiriki kutoka Timu ya Ofisi ya Rais Jiji Dodoma, Devotha Selufara, alisema amefurahishwa na kuwepo kwa michuano hiyo na kuomba michezo hiyo iwe endelevu ili kuendelea kuimarisha afya kimwili na kiakili. “Ninaomba zoezi hili lisiishie hapa, lijirudie ili tuwe tunafanya mazoezi mara kwa mara kwasababu ina imarisha viungo vyetu lakini pia afya zetu zinakuwa salama” alisema Selufara.

Nae, shabiki na mpenzi wa mchezo wa kuvuta kamba, Perpetua Mtega, aliwaasa washiriki wa michezo mbalimbali kutokuwa na tabia ya kukata tamaa hasa pale wanapopoteza katika michuano hiyo kwasababu katika mchezo wowote lazima apatikane mshindi na asiyekubari kushindwa siyo mshindani. “Nimefurahi kwa sababu wachezaji wote wamejiamini, wamejitoa na walikuwa tayari kupokea ushindi hivyo sina budi kusema kwamba popote kunapokuwa na ushindani lazima apatikane mshindi mmoja” alisema Mtega.

Ushindi wa wachezaji katika michezo mbalimbali hutegemea sana maandalizi mazuri ya awali, uthubutu, kujiamini na bidii ya kutosha ili kuepuka kuteteleka ndani ya mchezo.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.