• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

TAMISEMI yatangaza ajira kwa walimu 2,160

Imewekwa tarehe: August 21st, 2018

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR – TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo, ametangaza kuwapangia vituo vya kazi walimu wapya wa sekondari na mafundi sanifu wa maabara 2,160.

Akitangaza vituo vya kazi vya walimu hao jana Jijini Dodoma,  Waziri Jafo amesema walimu hao ni sehemu ya ajira za walimu 6,785 ambao Ofisi ya Rais - TAMISEMI ilipata kibali cha kuwaajiri kutoka Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora mwezi Mei mwaka huu, ambapo walimu 4,840 walipangiwa vituo vya kazi mapema mwezi Julai mwaka huu.

“Leo tunawatangazia ajira za watumishi 2,160 waliopangwa katika shule za Sekondari 1,721 ambapo kati yao, walimu 1,900 ni wa masomo ya Sayansi na Hisabati, walimu 100 ni wa Kiingereza na Fundi Sanifu Maabara ni 160”

Amesema watumishi hawa waliopangiwa vituo vya kazi wanatakiwa kuripoti katika Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri husika na baadaye kwenye shule kuanzia tarehe 23 Agosti, 2018 hadi Septemba 5, 2018, huku wakiwa na vyeti halisi vya kitaaluma, na cheti cha kuzaliwa.

Waziri Jafo amewaelekeza Wakurugezi wa Halmashauri ambazo zimepangiwa watumishi hao kuwapokea kwa kuzingatia kanuni na taratibu za utumishi wa Umma katika kukamilisha taratibu nyingine za ajira ya watumishi hao wapya.

Amewataka watumishi hao wapya kutochukua posho ya kujikimu bila kuripoti katika kituo cha kazi kwani watachukuliwa hatua za kisheria, wala hakutakuwa na kubadilisha kituo cha kazi kwa sababu yoyote ile, badala yake muda uliotolewa kuripoti ukipita, nafasi hiyo itachukuliwa na mtu mwingine mwenye sifa stahiki ambaye hakuchaguliwa. 

Kuona majina ya watumishi walimu wa shule za sekondari waliopangiwa vituo vya kazi Bofya kiunganishi hapa chini:

Orodha-ya-walimu-wa-ajira-mpya-masomo-wa-sayansi-hisabati-lugha-literature-in-english-na-fundi-sanifu-maabara

Chanzo: Tovuti ya Ofisi ya Rais TAMISEMI www.tamisemi.go.tz

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.