• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

PROF. MWAMFUPE AWATAKA HOMBOLO MAKULU KUMSHUKRU RAIS KWA KUPELEKA WATOTO SHULE

Imewekwa tarehe: December 1st, 2023

Na. Dennis Gondwe, HOMBOLO MAKULU

WANANCHI wa Kata ya Hombolo Makulu wametakiwa kumshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha watoto wao wanasoma kwa bidii katika shule iliyojengwa na serikali ya awamu ya sita katika kata hiyo.

Kauli hiyo ilitolewa na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe alipotoa salamu kwa wananchi wa Kata ya Hombolo Makulu jijini Dodoma katika ziara ya Kamati ya Siasa Mkoa wa Dodoma.

Prof. Mwamfupe alisema “wito wangu kwa wananchi wa eneo hili la Hombolo Makulu hatuna namna yoyote ya kufunga safari kwenda Dodoma au Dar es Salaam kumshukuru Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tumshukuru tukiwa hapahapa kwa kuhakikisha watoto wetu wanatumia miundombinu ya elimu iliyojengwa shuleni hapa. Kumbuka sisi katika misingi ya elimu bado hatupo katika namba nzuri, moja wapo ya sabau zilizochangia ni ukosefu wa miundombinu. Sasa miundombinu imejengwa, shule zipo hapa tulitegemea idadi kubwa ya watoto shuleni hapa itoke hapa katika kata hii”.

Mstahiki Meya aliitaka Kamati ya shule hakikisheni majengo yaliyopewa thamani yanatunzwa vizuri ili yadumu muda mrefu. “Walimu tunategemea watoto waliokuwa wanatembea umbali mrefu kiwango cha ufaulu kinakwenda kuongezeka” alisema Prof. Mwamfupe.

Nae Katibu wa CCM Mkoa wa Dodoma, Pili Mbaga aliwapongeza wananchi wa kata ya hombolo makulu kwa kuendelea kuchapa kazi na kuwaahidi kuwa serikali yao itaendelea kuwapelekea maendeleo.

“Leo tumepokea taarifa kuwa kata hii wamepata shilingi 95,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu ‘two in one’. Vilevile, wamepokea shilingi 216,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya kidato cha tano na sita. Mheshimiwa Diwani ametuambia wamepokea mradi wa Shule mpya ya Msingi Mayeto. Hizi zote ni juhudi za Rais wetu kuwapenda wananchi wake na kuwasogezea maendeleo” alisema Mbaga.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Hombolo Makulu, Gideon Nkana alimshukuru Rais kwa miradi ya maendeleo inayopelekwa katika kata yake. “Ninamshukuru sana Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo ametuheshimisha. Kata ya Hombolo Makulu ilikuwa ni miongoni mwa kata ambazo hazikuwa na miundombinu ya elimu ya sekondari. Ametutendea haki ametujengea shule kubwa lakini ametuletea madarasa nane kwa ajili ya kidato cha tano na sita” alisema Nkana.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.