• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Prof. Mwamfupe Mstahiki Meya tena Jiji la Dodoma, Mafuru aahidi kazi

Imewekwa tarehe: December 10th, 2020

BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma leo tarehe 10 Disemba, 2020 limefanya Mkutano wa kwanza katika ukumbi mkuu wa Halmashauri hiyo na kumchagua Diwani wa Kata ya Madukani kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Prof. Davis Mwamfupe (pichani juu) kwa jumla ya kura 54 kati ya 54 zilizopigwa, hivyo kumfanya kushinda tena kiti cha Meya wa Halmashauri ya Jiji hilo kwa muhula mwingine wa miaka mitano.

Aidha Baraza hilo limemchagua Diwani wa Kata ya Matumbulu Mhe. Emmanuel Chibago kuwa Naibu Meya, kwa kura 54 kati ya 54 zilizopigwa.

Akiongea baada ya ushindi huo, Mhe. Prof. Mwamfupe alitoa shukrani za dhati kwa Chama chake na Madiwani wote waliomuamini na kumpigia kura na kuahidi kushirikiana nao katika kuwatumikia wananchi wa Jiji la Dodoma kwa lengo la kuwaletea maendeleo.

"Niwashukuru sana waheshimiwa Madiwani kwa kunichagua, ninachokiomba kwenu ni ushirikiano, tukishirikiana hakuna jambo litakalotupa shida, nawashukuru viongozi kwa kusimamia kanuni, na ninaahidi kuongoza kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa bila ubaguzi wala upendeleo wa aina yoyote." Alisema Prof. Mwamfupe.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mhe. Josephat Maganga alisema kuwa uchaguzi umeisha na kazi inayofuata ni ya Madiwani kutekeleza wajibu wao kwa mujibu wa sheria kanuni na maelekezo.

Maganga amewaomba waheshimiwa Madiwani hao kujadili mambo yatakayoleta tija katika Kata zao na Jiji kwa ujumla kama vile masuala ya miundombinu ya barabara, afya na elimu, na yeye kama Mkuu wa Wilaya atakuwa mstari wa mbele kuwapa ushirikiano katika utekelezaji wa masuala yatakayoleta maendeleo Jijini hapa.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Joseph Mafuru alimpongeza Meya na Naibu wake kwa ushindi wa kishindo pamoja na waheshimiwa Madiwani na kuwahakikishia kuwa yale yote watakayokua wanajadiliana kwenye vikao watayatekeleza kwa wakati na kwa ufanisi wa hali ya juu.

"Mimi na timu yangu niwaahidi kitu kimoja kuwa tupo tayari kushirikiana nanyi waheshimiwa Madiwani ili kuleta maendeleo katika Jiji letu la Dodoma kwani kazi yetu kubwa ya kwanza ni kutoa huduma kwa wanachi wetu kama Halmashauri nyingine, lakini pili tunakazi ya kustawisha Makao Makuu ya nchi hivyo tukishirikiana tutawaletea maendeleo wananchi wetu na Taifa kwa ujumla." Alisema Mafuru.

Mhe. Prof. Devis Mwamfupe na Mhe. Emmanuel Chibago (kushoto) kabla ya uchaguzi ambapo wote wamechaguliwa na Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuendelea na vyadhifa walizokuwa wakizishikilia kabla ya Uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Mhe. Josephat Maganga akitoa nasaha zake mbele ya Madiwani (hawapo pichani).


Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru akiongea kutoa ahadi ya timu yake ya menejimenti kutoa ushirikiano kwa madiwani ili kuhakikisha Jiji linazidi kupiga hatua katika maendeleo.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.