• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Prof. Mwamfupe:Wanaonyanyasa Wanawake, Watoto 'kusakwa'

Imewekwa tarehe: February 20th, 2019

SHIRIKA la Wanawake la Umoja wa Mataifa (UN Women) kwa kushirikiana na Jumuiya ya Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT) wanatekeleza mradi wenye lengo la kutokomeza ukatili na unyanyasaji wa kijinsia kwa Wanawake na Watoto  wenye umri wa kati ya  miaka 15  hadi 49 katika maeneo ya wazi na mikusanyiko kama Masoko, Baa, Shule, na Taasisi mbalimbali za Umma  ambapo suala la wanawake kushikwa bila ridhaa yao linaelezwa kama kikwazo na changamoto kubwa.

Akifungua warsha ya siku moja ya kuhamasisha  jamii kuhusu jitihada za kuzuia na kupambana na unyanyasaji huo katika ukumbi wa Jiji jana, Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji  la Dodoma Profesa Davis Mwamfupe alisema Wanawake na Watoto wanafanyiwa matukio mengi ya kikatili kama vile kushikwashikwa miili yao na kuzomewa kwa sababu ya maumbile yao.

 Alisema kwa sasa kumekuwa na ongezeko kubwa la vitendo visivyofaa katika jamii ikiwemo ulevi uliopindukia, utumiaji wa dawa za kulevya hasa bangi, ukabaji na uporaji pamoja na uvaaji wa mavazi yasiyozingatia maadili na kwamba vyote hivyo vinachangia katika ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto.

“Tutambue kuwa wanawake na watoto wanakutana na matukio mengi ya ukatili, unyanyasaji, na kufanyiwa vitendo visivyofaa…hili linathibitishwa na tafiti mbalimbali ikiwemo ule wa ‘Tanzania Demographic Survey’ wa mwaka 2015/2016  unaoonyesha kuwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwa Wanawake na Watoto wenye  umri wa kati ya  miaka 15 hadi 49 umefikia Asilimia 40” alisema Mwamfupe katika hotuba yake.

Aidha, Mwamfupe alisema kuwa wanawake wengine wanadhalilishwa kutokana na maumbile yao, jambo ambalo ni kikwazo kwa uhuru dhidi yao, na kwamba ni wakati kwa jamii nzima kupaza sauti ya kupambana na hali hii kwani athari zake ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ya Wanawake na Watoto ikiwemo kupata fursa za Elimu na kushiriki katika shughuli za kiuchumi.

Akizungumza wakati wa warsha hiyo, Ofisa Maendeleo ya Jamii Mkuu kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI Mwajina Lipinga alisema kuna haja ya kuweka Sheria ndogo zitakazoshughulikia matukio kama haya.

“Tuna haja ya kufikiria tuweke Sheria ndogo ambazo zitasaidia kudhibiti kwenye haya maeneo kuzuia vitendo vya ukatili visitokee na kudhibiti pale yanapotokea” alisema Mwajina.

Mradi huo ambao unatarajiwa kupambana na hali hiyo, unatekelezwa katika Mikoa ya Dodoma na Shinyanga kama maeneo ya kuanzia, ambapo warsha ya uhamasishaji ilijumuisha baadhi ya Madiwani, baadhi ya Maofisa Watendaji wa Kata, Baadhi ya Wakuu wa Idara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Baadhi ya Maofisa Maendeleo ya Jamii ngazi ya Kata, Wawakilishi wa Wanawake wanaofanya biashara katika Masoko, Viongozi wa Masoko, na Wawakilishi wa vikundi vya Wanaume wanaofanya biashara katika Masoko.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.