• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais aapisha mabalozi watano Ikulu ya Chamwino

Imewekwa tarehe: November 23rd, 2019

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amewapa wiki moja mabalozi aliowateua na kuwaapisha leo, wawe wamewasili vituo vyao vya kazi katika nchi wanazowakilisha na kuchapa kazi.

Kauli hiyo ameitoa muda mfupi baada ya kuwaapisha katika Ikulu ya Chamwino iliyopo Dodoma leo asubuhi.

Rais Dkt. Magufuli ametoa wiki moja kwa mabalozi hao kuwa wameondoka Tanzania kwenda kufanya kazi katika nchi walizopangiwa. Kauli hiyo inafuatia tabia iliyokuwa ikifanywa na baadhi ya mabalozi wanapoapishwa badala ya kwenda katika nchi walizopangiwa wanatumia muda mrefu nchini kabla ya kuondoka.

Wakati huohuo, Rais amewapongeza mabalozi hao ambao ni mabalozi wa kwanza kuapishwa Ikulu ya Chamwino Dodoma na kutaka utendaji kazi wao ukaakisi Makao Makuu ya nchi. “Nendeni mkamtangulize Mungu katika kazi zenu, nawatakia mafanikio mema” alimalizia Rais.

Katika hatua nyingine, Waziri mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amewataka mabalozi walioapishwa leo kutambua kuwa Tanzania ina maslahi katika nchi wanazokwenda kuwakilisha. Aliwakumbusha kuwa dhamira ya nchi ni kufikia uchumi wa viwanda. “kupitia nyie tunaamini nchi hizo zitakwenda kuchangia katika uchumi wa viwanda. Nchi mnazokwenda kuna watanzania walio huko. Mkawatambue ili nao wahamasishwe kuisemea nchi yetu, kuilinda na kuitetea nchi yetu. Tunahitaji mchango wao ili kuimarisha maslahi ya nchi yetu” alisema Waziri mkuu Majaliwa.

Kwa upande wake, Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika mashariki Prof. Palamagamba Kabudi amewataka mabalozi walioapishwa leo kutunza uaminifu na imani ambayo Rais Dkt. John Magufuli amewapa. “Msivunje viapo vyenu na msiwe legelege” alisema Prof. Kabudi.

Naye Rais Magufuli, katika maneno machache aliyoyatoa baada ya hotuba ya Waziri Kabudi, alisema: “Najua mengi yameshasemwa, kwa kifupi napenda kuwapongeza mabalozi niliowaapisha leo, mkaiwakilishe nchi yetu vizuri na nawapongeza kwa kuwa ndiyo mabalozi wa kwanza kuapishwa hapa Ikulu ya Dodoma” amesisitiza Rais Magufuli.

Mabalozi walioapishwa na nchi zao kwenye mabano ni Balozi Maj. Gen Anselm Shigongo Bahati (Misri), Balozi Mohamed Abdallah Mtonga (Abu Dhabi), Balozi Jestas Abouk Nyamanga (Ubelgiji), Balozi Ali Jabir Mwadini (Saud Arabia) na Balozi Dkt. Jilly Elibariki Malebo (Burundi).



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.