• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Magufuli aapishwa, aahidi makubwa, Jiji la Dodoma lazizima

Imewekwa tarehe: November 5th, 2020

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli aahidi kuendelea kukuza uchumi na kukabiliana na tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana, muda mfupi baada ya kula kiapo (pichani) kwa nafasi ya urais tukio lililofanyika katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma leo.

Rais, Dkt Mafuguli amesema kuwa jukumu alilonalo ni kukuza uchumi wa Watanzania na kukabiliana na ukosefu wa ajira kwa vijana. “Serikali ninayoiongoza itazidisha mapambana dhidi ya rushwa, wizi na ubadhirifu wa mali ya umma” alisema Dkt. Magufuli.

Aidha, ameahidi kujenga uwanja mkubwa wa kisasa wa michezo jijini Dodoma.  “Shukrani sana wana Dodoma kwa kuhudhuria kwa wingi kwenye tukio hili. Watu wameanza kuingia uwanjani usiku, nawashukuru kwa heshima hii kubwa mliyonipa na imedhihirisha kuwa Dodoma ndiyo Makao Makuu ya nchi. Serikali itakayoanza leo, kitu cha kwanza ni kujenga uwanja mkubwa wa michezo hapa Dodoma ili sherehe zijazo watu wote wa Dodoma wawe ndani ya uwanja washerehekee vizuri” alisema Rais, Dkt. Magufuli.

Amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi kimepata ushindi mkubwa kutokana na baraka za wana Dodoma kwa sababu uzinduzi na kilele cha kampeni za uchaguzi mkuu zilifanyika Jijini Dodoma. “Yote tuliyoahidi tutayashughulikia ikiwemo ujenzi wa barabara ya mzunguko, sababu msongamano umeanza kuonekana Dodoma” aliongeza Rais huyo.

Akitoa salamu kwa niaba ya wananchi wa Jamhuri ya Comoro, Rais wa nchi hiyo, Azali Assoumani alimuomba Mungu kumsaidia sana Rais, Dkt. Magufuli kutekeleza kazi aliyopewa na watanzania kwa ufanisi.

“Nachukua nafasi hii kuwapongeza wananchi wa Tanzania kukamilisha salama mchakato wa uchaguzi, nawashukuru kwa uwepo wao hapa. Tunashukuru kila tunapokuja Tanzania mimi na ujumbe wangu tunapokelewa vizuri na kujisikia tupo nyumbani” alisema Rais Assoumani.

Nae, Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa alisema “naleta salamu nyingi kutoka kwa wananchi wa Zimbabwe. Tunamshukuru Rais, Dkt. Magufuli alifanya ziara nchini Zimbabwe. Na wakati wa ukame mkali, Rais Dkt. Magufuli alitupatia msaada wa mahindi kwa Wazimbabwe. Huyu ni kiongozi mzalendo katika ukanda huu”.

Wakati huohuo, Mwanazuoni na Mhadhiri wa Sheria kutoka Kenya, Prof. Patrick Loch Otieno Lumumba kupitia televisheni ya TBC amempongeza Rais, Dkt. Magufuli na CCM kwa ushindi mkubwa katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Prof. Lumumba ametoa tahadhari kuwa makini na wafadhili wavurugaji nchi za kiafrika. “Katika nchi za kiafrika, tuwe wepesi kujiepusha na wafadhili wenye lengo la kuvuruga nchi za Afrika. Tatizo la nchi za Afrika ni kutotofautisha upinzani na ubabaishaji. Tuhakikishe tunaendesha siasa ambazo zinalinda usalama wetu” amesema Prof. Lumumba kwa msisitizo.

Rais, Dkt. John Pombe Magufuli ameapishwa leo katika sherehe za aina yake zilizofanyika kwa mara ya kwanza Jijini Dodoma katika uwanja wa Jamhuri tangu Dodoma kupata hadhi ya Jiji na kuwa Makao Makuu ya nchi.

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan akila kiapo kushika nafasi hiyo kwa miaka mingine mitano.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.