• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Magufuli amuapisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Mawaziri wengine 2

Imewekwa tarehe: November 16th, 2020

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 16 Novemba, 2020 amemuapisha Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mhe. Rais Magufuli pia amewaapisha Mawaziri 2 aliowateua hivi karibuni katika Baraza lake jipya la Mawaziri ambao ni Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi aliyeapishwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Dkt. Philip Isdor Mpango aliyeapishwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango.

Halfa ya uapisho huo imefanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Hussein Ali Mwinyi, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma, Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Tulia Ackson.

Wengine ni Mawaziri Wakuu Wastaafu, Maspika Wastaafu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Adelardus Kilangi, Viongozi Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Wakuu wa Mikoa, Makatibu Wakuu, Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, viongozi wa Dini, viongozi wa Vyama vya siasa pamoja na viongozi na watumishi wa Taasisi na Idara mbalimbali za Serikali.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Rais Magufuli amewataka Wabunge kutulia wakati akiendelea na mchakato wa uteuzi wa Mawaziri watakaounda Baraza la Mawaziri kwa kuwa ameamua kupitia kwa umakini mkubwa orodha ya Wabunge wote takribani 350 ili kupata wachache atakaowateua kuwa Mawaziri.

Mhe. Rais Magufuli ameeleza dhamira yake ya kutaka Serikali ifanye kazi zaidi katika kipindi chake cha pili cha uongozi kwa kuwa anatambua kuwa Watanzania wana imani na matumaini makubwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho wamekichagua kwa ushindi mkubwa na wa kihistoria kwa Tanzania Bara na Zanzibar, hivyo anataka viongozi ambao atawateua wawe na uwezo wa kweli wa kutimiza matarajio hayo ya wananchi.

Kuwa upande wake, Mhe. Waziri Mkuu Majaliwa amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa imani kubwa aliyoiondesha kwake na ameahidi kutekeleza wajibu wake kwa nguvu zaidi pamoja na kumshauri ipasavyo, na kwa kuanzia ameahidi kuchukua hatua mara moja dhidi ya upandishaji wa bei ya Saruji uliojitokeza siku chacha zilizopita.

Halil kadharika, Mhe. Waziri Kabudi na Mhe. Waziri Mpango wameahidi kutekeleza wajibu wao kwa nguvu zaidi na kwa kugusa zaidi mahitaji ya wananchi, hasa baada ya kupata uzoefu wakati wakigombea katika majimbo ambako wamechaguliwa kuwa Wabunge katika uchaguzi mkuu uliopita.

Chanzo:Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU Gerson Msigwa - Chamwino



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.