• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Magufuli atoa shilingi Bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa

Imewekwa tarehe: November 26th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametoa shilingi Bilioni 10 kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa katika eneo la Kikombo Jijini Dodoma.

Mhe. Rais Magufuli ametoa fedha hizo jana tarehe 25 Novemba, 2019 baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi huo na ameagiza milima yote inayozunguka eneo la Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa lenye ukubwa wa ekari 5,567 imilikiwe na JWTZ kwa ajili ya shughuli za ulinzi.

Kuhusu madai ya fidia, Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Bw. Godwin Kunambi kuwalipa fidia ya shilingi Bilioni 3 na Milioni 339 wananchi 1,500 wa Kata ya Kikombo ambao ardhi yao imechukuliwa na JWTZ kwa ajili ya Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa, kuanzia tarehe 01 Desemba, 2019.

Pamoja na agizo hilo, Mhe. Rais Magufuli amewatahadharisha wananchi wa Kikombo kujiepusha na matapeli wanaowahamasisha kudai fidia wasiyostahili kwa mujibu wa sheria ama kudai ardhi isiyo yao.

Mhe. Rais Magufuli pia ameiagiza Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kujenga kwa kiwango cha lami kilometa 18 za barabara inayounganisha Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa na barabara kuu ya Dodoma – Morogoro.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amekubali ombi la Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jen. Venance Salvatory Mabeyo aliyeomba Serikali ibebeba jukumu la kulipa deni la takribani shilingi Trilioni 1 ambalo JWTZ inadaiwa baada ya kujengewa nyumba 6,064 za makazi ya Askari katika maeneo mbalimbali nchini, badala ya Askari kukatwa posho zao ili kupata fedha za kulipia deni hilo kama ilivyowekwa katika mkataba wa ujenzi.

“Nakuhakikishia hakuna kukatwa Askari yeyote, hilo deni litabebwa na Serikali, kabla sijaja hapa nimeshamwelekeza Waziri wa Fedha na Katibu Mkuu, na nafikiri kesho au keshokutwa wataanza kulipia hilo deni ambalo limeanza kuiva, tutaanza kulipa Dola za Marekani zaidi ya Milioni 25 (sawa na shilingi Bilioni 56 na Milioni 948). Mkataba ni kweli ulikosewa, nafikiri ilikuwa ni mwaka 2012/13 lakini siwezi kukubali makosa ya namna hiyo yakafanyika katika kipindi changu”amesema Mhe. Rais Magufuli.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewapongeza Maafisa na Askari wa JWTZ kwa kazi nzuri ya kulinda mipaka ya nchi na kushiriki katika operesheni za kulinda amani katika Mataifa mbalimbali, majukumu ambayo yamelijengea heshima jeshi hilo na Tanzania.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jen. Venance Salvatory Mabeyo wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa maelekezo yake ya kujengwa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa katika eneo la Kikombo ambayo yanajengwa na jeshi lenyewe.

Mapema kabla ya kuweka jiwe la msingi la mradi huo, Mhe. Rais Magufuli ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa uwanja wa maadhimisho ya kitaifa katika eneo la Chamwino.

Ujenzi wa uwanja huo utakamilika Januari 2020 ukiwa na uwezo wa kuchukua watu 5,000 kwa gharama ya shilingi Bilioni 2, na awamu ya pili itahusisha ujenzi wa ukumbi wa mikutano, jengo la watu mashuhuri na jengo la kupumzikia watu.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.