• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Magufuli azindua Mji wa Serikali - Mtumba

Imewekwa tarehe: April 13th, 2019

RAIS Mhe. John Magufuli amezindua rasmi Mji wa Serikali Mkoani Dodoma ambao ni Makao Makuu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Jumamosi Aprili 13 ambapo amewataka watumishi wa Wizara za Serikali kuhakikisha wanaanza kutumia Ofisi hizo kuanzia Jumatatu Aprili 15.

Katika uzinduzi huo uliofanyika katika eneo la Mtumba (umbali wa kilometa 17 kutoka katikati ya Jiji la Dodoma) Rais Magufuli amewataka wakazi wa Dodoma na watanzania kwa ujumla kutumia fursa hiyo kukuza uchumi wa nchi kwa kuwekeza katika biashara mbalimbali.

“Ninawasihi Watanzania kwa ujumla kutumia fursa ya serikali kuhamia Dodoma, kama mlivyosikia zimetolewa ajira 1,288 na fursa bado zipo kama vile shule, hospitali, migahawa, kilimo na hoteli...mmeshaona Mabalozi wameshahamia hivyo tuzitumie hizi fursa kuleta maendeleo na kuijenga Dodoma ya kisasa,” alisema.

Katika hatua nyingine Mhe. Rais Magufuli amempandisha cheo aliyekuwa Luteni Kanali, Charles Mbuge kuwa Brigedia Jenerali baada ya kufurahishwa na utendaji wake wa kazi katika kusimamia ujenzi wa miradi mbalimbali ya Serikali ikiwemo ujenzi wa ukuta wa Mererani, nyumba za Serikali, nyumba za Magereza na Ofisi za Wizara kwenye Mji wa Serikali, huku akikubali ombi la kuwaajiri vijana wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) walioshiriki katika kazi ya ujenzi kwenye operesheni kadhaa ambapo alisema idadi kubwa wataenda Jeshi la Wananchi, na wengine TAKUKURU, UHAMIAJI, POLISI, na TISS.

“Ninawapongeza maofisa walioshiriki kukamilisha mradi huu na Kanali Mbuge alisimamia ujenzi wa majengo mbalimbali ya Serikali pamoja na ukuta wa Mererani hivyo kuanzia leo nampandisha cheo atakuwa Brigedia Jerenali, sitaki kuchelewa hivyo ninataka Mkuu wa Majeshi (CDF) ukafanye utaratibu wa vile vinavyotakiwa kuwekwa kwenye mabega awekewe” alisema.

Aidha, Rais Magufuli alizipongeza taasisi mbalimbali ikiwemo Halmashauri ya Jiji la Dodoma, zilizoshiriki katika mchakato wa kufanikisha ujenzi wa Mji huo wa serikali katika eneo la Mtumba na kupongeza umoja, upendo na ushirikiano uliopo kati ya viongozi wa Wilaya na Jiji la Dodoma.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.