• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Magufuli ziarani Jijini Dodoma

Imewekwa tarehe: November 20th, 2019

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli anatarajiwa kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani Dodoma kutembelea miradi ya maendeleo.

Akiongea na waandishi wa habari wa Mkoa wa Dodoma ofisini kwake leo, Mkuu wa Mkoa huo, Dkt. Binilith Mahenge alisema kuwa ziara hiyo itaanza tarehe 21 hadi 25 Novemba, 2019.

Dkt. Mahenge alisema “natumia fursa hii kuwatangazia wananchi wote wa Mkoa wa Dodoma na umma wa watanzania kuwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt. John Pombe Magufuli, imempendeza kufanya ziara ya kikazi katika Mkoa wa Dodoma, makao makuu ya nchi, kuanzia tarehe 21-25 Novemba, 2019. Katika ziara hiyo atatembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Mkoa wa Dodoma na kuzungumza na wananchi”.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma alizitaja shughuli zitakazofanywa na Rais kuwa, tarehe 21 Novemba, 2019 Mhe Rais atakuwa mgeni rasmi katika mahafali ya 10 ya chuo kikuu cha Dodoma. Tarehe 22 Novemba, 2019 Mhe Rais atatembelea na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi ya hospitali ya Uhuru, wilayani Chamwino; ujenzi wa nyumba 118 za askari Polisi katika maeneo ya FFU Nzuguni na Medeli East; ujenzi wa stendi kuu ya mabasi iliyopo Nzuguni; na soko kuu linalojengwa eneo la Nzuguni. Siku hiyo itahitimishwa na mkutano wa hadhara utakaofanyika katika stendi ya mabasi Nzuguni na kurushwa moja kwa moja na vyombo mbalimbali vya habari.

Katika siku ya tatu ya ziara hiyo tarehe 25 Novemba, 2019, Mhe Rais ataweka mawe ya msingi kwenye miradi ya ujenzi wa makao makuu ya Jeshi la wananchi wa Tanzania eneo la Kikombo; ujenzi wa ofisi ya makao makuu ya idara ya Uhamiaji na ujenzi wa jengo la makandarasi katika eneo la National Capital City.

Akiongelea maandalizi ya ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa alisema kuwa maandalizi yamekamilika. “Ziara ya Mhe Rais kwetu ni fursa ya kumuonesha hatua tulizofikia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo aliyotupatia na kupokea maelekezo ya namna ya kusonga mbele kwa uhakika katika hatua mbalimbali za utekelezaji wake” alisema Dkt. Mahenge.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.