• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Mhe. Magufuli azindua mradi wa maji Kibamba - Kisarawe

Imewekwa tarehe: June 28th, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 28 Juni, 2020 amezindua mradi wa maji wa Kibamba - Kisarawe ambao unatekelezwa kufuatia maelekezo aliyoyatoa tarehe 21 Juni, 2017.

Sherehe za uzinduzi wa mradi huo zimefanyika Kisarawe Mkoani Pwani na kuhudhuriwa na wananchi na viongozi mbali mbali wakiwemo Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu, Viongozi wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, viongozi wa Dini na viongozi wa Mkoa wa Pwani wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhandisi Evarist Ndikilo.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazinginra Dar es Salaam (DAWASA) ambayo ndio imetekeleza mradi huo Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema  mradi huo wenye mtandao wa Kilometa 15.65 za bomba kuu, kilometa 48 za mabomba ya usambazaji, matenki mawaili ya lita Milini 6.5 na pampu 2 umejengwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 1.6 ambapo fedha zote zimetokana na makusanyo ya ndani ya DAWASA.

Mradi huo unawanufaisha wananchi wa Kata za Kisarawe, Kazimzumbani, Masali, Kibuta, Kiluvya, Kwemba, Kisopwa na Mloganzila. Pia DAWASA inapanua mradi huo kwa shilingi Bilini 7.7 ili uwafikie wananchi wa Pugu, Gongolamboto, Ukonga, Airwing, Banana, Mongolandege, Kinyerezi, Chanika na Segerea ambapo utanungana na mradi wa maji wa Ruvu Juu na Ruvu Chini.

Waziri wa Maji Prof. Makame Mbarawa amemueleza Mhe. Rais Magufuli kuwa pamoja na kutekeleza agizo hilo, Wizara ya Maji imetekeleza agizo lake la kuhakikisha ukusanyaji wa mapato ya maji unaogezeka ambapo DAWASA imeongoza ukusanyaji wa mapato hayo kutoka shilingi Bilioni 2.9 kwa mwezi (mwaka 2018) hadi kukfikia shilingi Bilioni 12.3 (mwaka 2020) na kwamba kazi kama hiyo inafanyika nchi nzima ambapo miradi 192 yenye thamani ya shilingi Bilinii 163.78 inatekelezwa kwa utarativu wa 'Force Account' ambapo Serikali itaokoa zaidi ya shilingi Bilioni 48.73 ikilinganishwa na endopo itawatumia wakandarasi.

Mhe. Rais Magufuli ameipongeza DAWASA kwa utekelezaji mzuri wa mradi huo, kuongeza ukusanyaji wa mapato na kuwa na mpango mzuri wa upanunzi wa mtandao wa maji, hivyo ameitaka Menejimenti ya DAWASA kuboresha maslahi ya wanafanyakazi wake.

Mhe. Rais Magufuli pia ameipongeza Wizara ya Maji kwa utekelezaji wa miradi wa maji nchini ambapo katika kipindi cha miaka 5 miradi 1,423 imetekelezwa hapa nchini kwa gharama za shilingi Trilioni 3 na  kwamba kutokana na juhudi hizo za Serikali hali ya upatikanaji wa maji nchini imeongezeka kutoka wastani wa asilimia 47 hadi 70.1 (Vijijini) na wastani wa silimia 74 hadi 84 (Mijini).

Katika sherehe hizo, Mhe. Rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kuanza mchakato wa ujenzi wa barabara ya lami kuunganisha Kisarawe na Hifadhi ya Taifa ya Nyerere na ameiagiza Wizara ya Nishati kuongeza kiwango cha umeme katika Mkoa wa Pwani ili kukidhi mahitaji yote ya kilowati 73 badala ya hali ya sasa ambapo mkoa huo unapata kilowati 30.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Kapteni Mstaafu George Mkuchika kutengua uteuzi wa Bw. Mtera Mwampamba aliyekuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisalawe kutokana na kashfa mbalimbali na ameagiza Bi. Mwanana Msumi ateuliwe kushika wadhifa huo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akivuta utepe pamoja na Waziri wa Maji Profesa Makame Mbarawa ili kuzindua mradi mkubwa wa maji wa Kibamba-Kisarawe katika sherehe zilizofanyika Wilayani Kisarawe Mkoani Pwani tarehe 28 Juni, 2020.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akifungua maji kwenye eneo la mradi wa Kibamba-Kisarawe mkoani Pwani mara baada ya kuzindua mradi huo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akishika maji ya bomba mara baada ya kuzindua mradi wa maji wa Kibamba-Kisarawe.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na viongozi wengine wakifungua maji kwa pamoja kwa furaha.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.