• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Samia ahutubia kilele cha wiki ya Sheria Chinangali Park Dodoma

Imewekwa tarehe: February 2nd, 2022

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, ametoa wito kwa Sekta ya Sheria na Utoaji wa Haki nchini kuangalia namna bora ya kutayarisha wahitimu na kuongeza maarifa kwa wanasheria walio kazini yaendane na wimbi la ukuaji wa teknolojia ya TEHAMA, ili nchi iweze kunufaika na matumizi ya teknolojia hiyo. 

Mhe. Rais Samia ametoa wito huo leo tarehe 02 Februari, 2022 wakati akihutubia katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Jijini, Dodoma.

Aidha, Mhe. Rais Samia amesema kuwa dunia ipo kwenye Mapinduzi ya Nne ya Viwanda ambayo yanaongozwa na sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), hivyo uchumi wa dunia pamoja na shughuli mbalimbali zinaendeshwa kwa kutumia TEHAMA.

Mhe. Rais Samia amezitaka Wizara za Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Vyuo Vikuu vyote kuhakikisha kuwa wanafunzi kuanzia shule za msingi hadi vyuo vikuu wanapatiwa ujuzi utakaowaandaa kufanya kazi zinazohitaji ujuzi unaolingana na matakwa ya mabadiliko ya teknolojia. 

Pia, Mhe. Rais Samia amesema wakati tulionao unahitaji mabadiliko makubwa ya kifikra na kuzalisha nguvu kazi yenye ujuzi linganifu na mabadiliko ya teknolojia duniani. 

Mhe. Rais Samia amewapongeza viongozi wa sekta ya Sheria kwa hatua zinazochukuliwa ikiwemo kutafuta teknolojia yenye programu za kisasa ambazo zitaimarisha matumizi ya lugha ya Kiswahili katika kutoa huduma za kimahakama na kutoa nafasi kwa lugha ya Kiswahili kupata tafsiri na unukuzi (transcription) kwa lugha ya Kiingereza na lugha zingine za kigeni. 

Vilevile, Mhe. Rais Samia amesema Serikali ipo tayari kutumia njia za kisasa katika kujenga uwezo na uchumi imara unaoweza kukabiliana na ushindani katika masoko ndani ya Kanda zetu za Afrika na Duniani kwa ujumla. 

Amesema, Tanzania haiwezi kubaki nje ya Mapinduzi ya Nne ya Viwanda ambayo yanaendelea kubadilisha mizani ya ushindani katika shughuli zote za kibinadamu, zikiwemo za uwekezaji na mazingira ya biashara. 

Mhe. Rais Samia amesema ili kufanikisha lengo hilo ni lazima kuiboresha sekta ya Sheria na Utoaji wa Haki nchini, ili iweze kukabiliana na migogoro na mashauri ya kibiashara, na kutoa ufafanuzi wa kisheria katika masuala ya uwekezaji na biashara wakati wowote.

Aidha, Mhe. Rais Samia ametoa wito kwa Mahakama kuzingatia Sheria na Katiba ya nchi na kutenda haki kwa watu wote bila kujali hali ya mtu kijamii au kiuchumi bila kucheleweshewa au kunyimwa haki wananchi kwa kufungwa na masharti ya kiufundi. 


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.