• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Samia ahutubia siku ya Mashujaa Dodoma

Imewekwa tarehe: July 25th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

SERIKALI ya awamu ya sita itaendelea kulijenga Jiji la Dodoma ili liwe la kisasa na lenye hadhi ya makao makuu ya nchi.

Kauli hiyo ilitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi waliojitokeza katika maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya Mashujaa iliyofanyika kitaifa katika uwanja wa Mashujaa jijini Dodoma.

Rais Samia Suluhu Hassan alisema kuwa mwaka 2016 katika uwanja wa Mashujaa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano, Hayati Dkt. John Magufuli alitangaza dhamira ya serikali kuhamia Dodoma. Alisema kuwa serikali itaendelea kuenzi maono ya muasisi wa taifa hilo Hayati Mwalimu Julius Nyerere ya kuhamishia makao makuu ya serikali Dodoma.

Akiongelea jitihada za kulijenga Jiji la Dodoma, alisema kuwa serikali yake inaendelea na awamu ya pili ya kujenga majengo ya kudumu ya wizara katika Mji wa Serikali na yanaendelea vizuri. Alisema kuwa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Msalato unaendelea kujengwa. Alisema kuwa serikali inaendelea kujenga na kuboresha miundombinu ya barabara katika jiji hilo. Jitihada nyingine alizitaja kuwa ni kupanda miti na kutunza usafi wa mazingira. “Ushujaa ni pamoja na kuiweka nchi katika uhakika wa chakula, elimu bora, umeme wa kutosha na maji” alisema Rais Samia.

Katika hatua nyingine Rais Samia alipendekeza Ofisi ya Waziri Mkuu kutafuta eneo kubwa na bora zaidi na kujenga Mnara wa Mashujaa wa makao makuu kwa gharama nafuu zinazokubalika.

Rais huyo alisisitiza wananchi kuendelea kuchanja chanjo dhidi ya UVIKO-19. Alisema kuwa kuchanja ni njia bora ya kulinda usalama wa taifa.

Vilevile, alikumbusha kuwa tarehe 23 Agosti, 2022 ni siku ya Sensa ya Watu na Makazi. Alisisitiza kila mwananchi amhimize mwenzake na kumwambia ushujaa ni kuhesabiwa.

Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2022 inaongozwa na kaulimbiu isemayo “Sensa kwa maendeleo, jiandae kuhesabiwa”.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama mbele ya mnara wa kumbukumbu ya mashujaa jijini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiweka ngao ya jadi kwenye mnara wa mashujaa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.