• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Samia apokea na kuizindua Ndege mpya ya 9

Imewekwa tarehe: July 30th, 2021

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 30 Julai, 2021 ameongoza Watanzania katika mapokezi ya Ndege mpya aina ya Bonbadier Dash 8-Q400 na kisha kuizindua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Kuwasili kwa Ndege hiyo iliyotokea nchini Canada kunaongeza idadi ya Ndege zilizonunuliwa na kuwasili kufikia 9 kati ya 11, Ndege nyingine 2 zinatarajiwa kuwasili mwezi Oktoba 2021.

Akizungumza wakati wa hafla ya kupoka Ndege hiyo, Mhe. Samia amesema usafiri wa anga ni kichocheo muhimu cha maendeleo duniain kwa sababau usafiri huo ni wa haraka, salama na wenye kutumiwa na watu wengi.

Mhe. Rais Samia amesema mbali na usafiri wa anga kusafirisha watu, pia ni muhimu katika kusafirisha bidhaa mbalimbali hususani zinazoharikiba haraka kama vile matunda, mbogamboga, samaki, maua, nyama na nyinginezo.

Amesema Serikali imeamua kununua Ndege ya kusafirisha mizigo kwa sababu nchi yetu ni mionognzi mwa wazalishaji wakubwa wa matunda, mbogamboga na maua ambapo mwaka 2019, Tanzania iliuza nje mazao yenye thamani ya takribani Dola za Kimarekani milioni 700 na inatarajia hadi kufikia mwaka 2025 kuingiza Dola za Marekani bilioni 2.

Aidha, Mhe. Rais Samia amesema ili nchi iweze kuvutia watalii wengi na kunufaika nao ni lazima iimarishe usafiri wa ang ana ndio sababu Serikali iliamua kufufua Shirika la Ndege la ATCL ikiwa na malengo ya kupokea watalii milioni 5 ifikapo mwaka 2025 katoka watalii milioni 1.5 mwaka 2019.

Amesema Serikali imeamua kuimarisha huduma za usafiri nchini ili iweze kunufaika na fursa za kijiografia za kupakana na nchi 8, ambapo kati ya hizo 6 hazina bandari.

Mhe. Rais Samia amezihimiza Wizara za Viwanda na Biashara, Wizara ya Uwekezaji na Sekta Binafsi kuweka mikakati ya kunufaika na fursa hizo ikiwemo kuanzisha kongani za kiuchumi kwenye maeneo ambapo miundombinu ya usafiri inajengwa.

Vile vile, Mhe. Rais Samia ameipongeza ATCL kwa kuimarika tangu ilipofufuliwa ambapo idadi ya watu wanaosafiri kwa Ndege za shirika hilo imeongezeka kutoka wastani wa abiria 4,000 hadi 60,000 kwa mwezi.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Shirika la ATCL Mhandisi Ladislaus Matindi amesema ATCL imeongeza safari za kimataifa kutoka kituo kimoja cha Comoro hadi saba ambavyo ni Burundi, China, India, Uganda, Zambia, Zimbabwe, Lubumbashi, Kalemie, Ndola, Nairobi, Dubai, Muscat na London.

Mapokezi ya Ndege hiyo mpya pia yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Mpango, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Hussein Katanga, Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Pamella O’Donell, viongozi wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Pamoja na viongozi mbalimbali wa dini na vyama vya siasa.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.