• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Samia azindua chuo cha VETA Kagera

Imewekwa tarehe: October 13th, 2022

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo amezindua Chuo Cha Ufundi Stadi na Huduma VETA Mkoa wa Kagera ambacho Ujenzi wake umegharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 22 ikiwa ni ufadhili kutoka Serikali ya China.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Rais Samia amemuelekeza Mkuu wa Mkoa wa Kagera Albert Chalamila, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa huo kuweka utaratibu mzuri wa kuhakikisha Asilimia 10 ya Fedha za mkopo kwaajili ya Vikundi vya Vijana kinamama na Wenye ulemavu zinawanufaisha pia wahitimu wa chuo hicho kwa kuwapatia fedha taslimu au kuwanunulia Vifaa na kuwatengea maeneo ili waweze kujiajiri.

Aidha Rais Samia amesema Chuo hicho kina uwezo wa kuchukuwa wanafunzi 1,400 wa mafunzo ya muda mrefu na muda mfupi ambapo ameahidi kukipatia chuo Shilingi Bilioni 1 kila mwezi kwaajili ya uendeshaji ili kupunguza makali ya ada huku akijitolea kusomesha Vijana 20 ambao familia zao hazina uwezo.

Ili kuhakikisha kila Wilaya inakuwa na chuo Cha VETA, Rais Samia amesema Serikali itaendelea kutenga Shilingi Bilioni 100 Kila mwaka kwaajili ya Ujenzi wa Vyuo hivyo na kuhakikisha Wilaya zote 62 ambazo hazina chuo Cha VETA zinakuwa na chuo hicho ikiwa ni pamoja na Ujenzi wa chuo Cha VETA Mkoa wa Songwe.

Rais Samia amesema lengo Ujenzi wa Vyuo hivyo ni kuongeza thamani na ujuzi kwa vijana wanaohitimu kuanzia Elimu ya Msingi mpaka chuo wapate ujuzi wa kuwasaidia kujiajiri wenyewe ili kukabiliana na tatizo la ukosefu wa ajira ambapo tafiti zinaonyesha Asilimia 12 ya Vijana hawana Ajira.

Kwa upande wake Balozi wa China nchini Tanzania, Balozi Cheng Mingjian amesema Ujenzi wa chuo hicho ni matokeo chanya ya ushirikiano baina ya Serikali ya China na Tanzania katika Mambo mbalimbali.

Chuo Cha VETA Mkoa wa Kagera kilichozinduliwa leo kina Madarasa 19 na Karakana 9 ambapo kitaanza kutoa Elimu mwezi January mwakani ambapo miongoni mwa masomo yatakayofundishwa ni Computer, ufundi wa umeme wa majumbani na viwandani, Ufundi Makenika, uchongaji vyuma, uchomeaji na uungaji vyuma, ufundi Bomba, ufundi umeme na mitambo, upakaji rangi, Ujenzi, ufundi seremala.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.