• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Rais Samia azindua kiwanda cha ushonaji cha Polisi

Imewekwa tarehe: May 19th, 2021

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 18 Mei, 2021 amefungua kiwanda cha ushonaji bohari kuu ya Jeshi la Polisi kilichopo Kurasini Mkoani Dar es Salaam.

Kiwanda hicho kimejengwa kwa utaratibu wa nguvu kazi (force account) kwa gharama ya shilingi Milioni 666.4 badala ya shilingi Bilioni 1.4 kama kingejengwa kwa utaratibu wa zabuni.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IJP Simon Sirro amesema ujenzi wa kiwanda hicho umepanua uwezo wa kiwanda kutoka vyerehani 70 hadi 130 vyenye uwezo wa kushona sare 125,000 za Askari kwa mwaka.

IJP Sirro amemshukuru Mhe. Rais Samia kwa kufungua kiwanda hicho na amesema Jeshi la Polisi linapanga kuanzisha shirika la uzalishaji litakaloendesha miradi mbalimbali kikiwemo kiwanda cha ushonaji, kiwanda cha kuzalisha maji na usindikizaji wa fedha.

Pia, IJP Sirro amemshukuru Mhe. Rais Samia kwa Serikali kutoa shilingi Bilioni 6 kwa ajili ya kuwalipa wastaafu wa Jeshi la Polisi ambao wameanza kulipwa.

Akizungumza na Maafisa wa Polisi, Askari na viongozi mbalimbali katika uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini, Mhe. Rais Samia amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kujenga kiwanda hicho kwa kutumia mapato yake ya ndani na kwa kutumia nguvukazi iliyotumia kiasi kidogo cha fedha ikilinganishwa na endapo lingetumia wazabuni.

Mhe. Rais Samia ameelezea kufarijika kwake kukifungua kiwanda hicho ambacho kiliwekwa jiwe la Msingi na aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na amesema kukamilika kwa kiwanda hicho ni uthibitisho wa kumuenzi Hayati Dkt. Magufuli.

Ameelekeza Majeshi mengine kushona sare zao katika kiwanda hicho na pia kujielekeza kushona sare nyingine kama vile viatu badala ya kila Jeshi kushona aina ileile ya sare zinazoshonwa na Jeshi lingine ili kudhibiti uagizaji wa sare za Askari kutoka nje ya nchi. 

Aidha, Mhe. Rais Samia amelitaka Jeshi la Polisi kujielekeza kudhibiti matukio ya uhalifu na uvunjaji wa sheria ikiwemo makosa ya usalama barabarani badala ya kujikita katika kutoa adhabu ama kuwa kitega uchumi.

Amelitaka jeshi hilo kuongeza juhudi katika kukabiliana na vitendo vya uhalifu ambavyo vimeanza kujitokeza na ameonya kuwa katika upandishaji wa vyeo, uteuzi na kutengua uteuzi wa Maafisa wakiwemo Makamanda wa Polisi wa Mikoa kipimo cha juhudi za udhibiti wa matukio ya uhalifu hasa ujambazi kitatumika.

Mhe. Rais Samia amelitaka Jeshi la Polisi kuweka mfumo utakaowezesha kutambuliwa kwa wavunja sheria za usalama barabarani popote walipo hapa nchini ili ikitokea dereva kafanya makosa katika mkoa mmoja aonekane katika mkoa mwingine na achukuliwe adhabu stahiki ikiwemo kufutiwa leseni.

Amelitaka Jeshi la Polisi kuendelea kupunguza msongamano wa Mahabusu waliokamatwa kutokana na makosa mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwaachia wenye kesi za kubambikizwa kama ambavyo imefanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambayo imefuta kesi 147 za rushwa za kubambikizwa.

Mhe. Rais Samia ameagiza sheria inayolazimu majeruhi kuwa na fomu ya PF3 ndipo wapatiwe matibabu katika vituo vya tiba irekebishwe ili majeruhi wasikoseshwe matibabu pale wanapokuwa hawana fomu hiyo.

Mhe. Rais Samia ameahidi kufanyia kazi changamoto mbalimbali za Jeshi la Polisi kadiri Serikali itakavyokuwa na uwezo wa kifedha.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.