• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RAS Dkt. Mganga aahidi makubwa Dodoma

Imewekwa tarehe: June 3rd, 2021

KATIBU TAWALA mpya wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Fatma Mganga, leo Juni 3, 2021 amepokewa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma na kuanza rasmi majukumu yake huku akiahidi utumishi uliotukuka katika kuwahudumia wananchi na kutatua changamoto zinazoukabili Mkoa wa Dodoma kwenye sekta za Elimu, Uchumi, Afya, Kilimo, Mifugo na huduma nyingine za jamii kwa ujumla.

Dkt. Mganga ameyasema hayo wakati wa hafla ya kumpokea iliyoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka wakati alipowasili kwa mara ya kwanza kama Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma kufuatia kuteuliwa kwake hivi karibuni na kuapishwa na Mheshimiwa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan Juni 2, 2021 kushika wadhifa huo.

Dkt. Mganga amesema kuwa yeye ni muumini wa kuibuka mshindi kwenye sekta zote muhimu anazozisimamia na hivyo amewataka watumishi wote wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Halmashauri za Mkoa wa Dodoma na Taasisi zote katika Mkoa huo kuwa na nidhamu, bidii na ubunifu katika kazi.

“Natambua Mkoa wa Dodoma unakabiliwa na changamoto ya Elimu na kwa muda mrefu Mkoa umekuwa na matokeo yasiyoridhisha katika mitihani ya Taifa huku ukishika nafasi ya 20 kushuka chini” Alisema Dkt. Mganga huku akiongeza kuwa ni jukumu la wanaDodoma wote kushirikiana na uongozi mpya wa Mkoa kuhakikisha hali hiyo inabadilika.

Akizigeukia Halmashauri za Mkoa wa Dodoma, Dkt. Mganga amesema kuwa anatambua changamoto zinazozikabili Halmashauri za Mkoa huo huku akiahidi kuzisimamia na kuzishughulikia akianzia na mgogoro unaoletwa na utofauti wa malipo ya waheshimiwa madiwani katika Halmashauri moja hadi nyingine za Mkoa wa Dodoma.

Aidha, ameahidi kuzisimamia kwa nguvu Halmashauri za Mkoa wa Dodoma kuhakikisha zinatenga asilimia 40% ya mapato yake na kupeleka kwenye miradi ya maendeleo na kupeleka asilimia 10% ya mapato ya ndani kwenye mikopo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka akitoa salamu za kumkaribisha Dkt. Mganga alisema kuwa, ana imani kubwa nae na kuwa amekuwa na utendaji uliotukuka uliopelekea kupanda madaraja kutoka mtumishi wa kawaida, Mkuu wa Idara, Mkurugenzi wa Halmashauri na hadi sasa ni Katibu Tawala wa Mkoa.

“Dkt. Mganga amekuwa na rekodi nzuri ya kiutendaji wakati akiwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi na Halmashauri hiyo wakati wa kipindi chake imekuwa Halmashauri ya mfano katika Mkoa wa Dodoma na maeneo mengine ya nchi, hivyo natarajia atayaendeleza hayo yote akiwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma” aliongeza Mhe. Mtaka.

Akimuwakilisha Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Dodoma Meja Mstaafu Risasi Salingwa, amesema kuwa ili Mkoa uweze kufanikiwa na kupiga hatua lazima viongozi wa Mkoa wa Dodoma wawe na sifa za kukubali kushauri na kushauriwa, waelewe hali ya wakati uliopo na aina ya wananchi wanaowaongoza, waongoze kwa mifano na matendo bora, watumie lugha thabiti ya kiungwana, wagawe madaraka kwa wasaidizi wao na kufuatilia mrejesho wa majukumu.

Aidha, waondoe ukabila, udini na makundi ya aina zote, wazuie migongano kwa kutumia njia ya vikao na majadiliano ya mikutano na wakumbuke kuwaendeleza watumishi kwa kuwapeleka masomoni, mafunzo, kutoa motisha ya kutambua utendaji wao na pia kuwapandisha vyeo na maslahi yao, alimalizia Mwenyekiti huyo.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.