• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RAS Dodoma awafunda watumishi wa Jiji

Imewekwa tarehe: June 17th, 2022

Na. Theresia Francis, Dodoma

KATIBU Tawala Mkoa wa Dodoma, Dkt. Fatuma Mganga (aliyesimama pichani juu) ameongea na watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuwakumbusha sheria za utumishi wa umma, uwajibikaji, utii na nidhamu mahala pa kazi.

Dkt. Mganga amekutana na watumishi hao leo katika ukumbi wa mikutano wa jiji hilo ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya serikali katika maadhimisho ya wiki ya utumishi wa umma.

“Tukiitumia wiki hii ya utumishi kwa umma vizuri tutaenda kutoa huduma nzuri kwa jamii, kila mmoja kwa nafasi yake Mungu amempa baraka ya kuwa mtumishi wa umma. Sisi ndio tunabeba taswira ya mkoa katika utumishi, matamanio ya serikali ni Dodoma kuwa sehemu bora katika kutoa huduma kwa umma. Tuwe na utayari wa kusaidia likilalamikiwa jiji imelalamikiwa Dodoma tuhakikishe wananchi na wageni wanapata huduma bora,“ alisema Dkt. Mganga.

Sambamba na hilo Dkt. Mganga alieleza kuhusu madhumuni ya wiki ya utumishi kwa umma kuwa ni kuboresha ufanisi wa kazi kwa kuhakikisha kiasi cha mshahara anachopokea mtumishi wa umma kinaendana na matokeo ya kazi yake. Dhumuni lingine alilitaja kuwa ni kuwakumbusha watumishi kanuni za utumishi wa umma, kuamsha ari ya utumishi bora na utoaji huduma pamoja na kutiana moyo .

Katibu Tawala huyo aliwaasa maafisa utumishi kuwa wabunifu na kutafuta mfumo wa kubaini watumishi wanaokuwa kero kwenye utumishi wa umma na wanao haribu taswira ya utumishi. “Ninategemea kupata mrejesho namna watumishi wanafanya kazi kwa kutumia mfumo taarifa ziwe kwa mtumishi mmoja mmoja namna anavyotoa huduma, kuwahi kazini, uwajibika nakadhalika ili tuweze kutoa huduma bora” alisisitiza Dkt. Mganga.

Kwa upande wake Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Utawala na Rasilimali watu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Aloyce Mwogofi aliwakumbusha watumishi misingi ya utumishi kuwa ni uwajibikaji, uadilifu kazini na kusimama kwenye nafasi kama watumishi wa umma. Nyingine ni kufanya kazi kwa bidii, kujitambua na kutunza rasilimali za serikali. Vilevile, aliwakumbusha kuwa na staha ili kutoa huduma nzuri kwa wateja na kuifanya Dodoma kuwa sehemu ya mfano katika utumishi wa umma.

Mwogofi alisema “watumishi wana wajibu wa kufanya kazi kwa uadilifu, mteja akija aone amefika kwenye kimbilio la tatizo lake na anapopata huduma akiondoka ashukuru na kuwataarifu wengine kwa huduma nzuri aliyoipata. Ifike mahali mteja awe na amani na uhakika wa kupata utatuzi anapokuja ofisini kwaajili ya kupata huduma”.

Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia Utawala na Rasilimali watu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Aloyce Mwogofi alipokuwa akingea na watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma leo tarehe 17 Juni, 2022 katika kuadhimisha wiki la utumishi wa umma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.