• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC aagiza Wakurugenzi kuvilipa vituo vya Afya

Imewekwa tarehe: November 27th, 2018

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote katika Mkoa huo kuhakikisha wanatumia bakaa ya fedha ya mwaka wa fedha uliopita (2017/2018) pamoja na fedha za Tele-kwa-Tele kulipa madeni yote kwenye vituo vya kutolea huduma za afya mkoani humo.

Alitoa maagizo hayo wakati wa kuzindua kampeni ya uhamasishaji wananchi kujiunga na mfumo wa bima ya CHF iliyoboreshwa Kimkoa iliyofanyika wilayani Mpwapwa.

Alisema agenda ya serikali ni kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora za afya kupitia mfumo wa CHF na kuziagiza Wilaya zote kufanya kampeni ya wananchi kujiunga na CHF iliyoboreshwa. 

“Hakikisheni viongozi wa serikali za mtaa na vijiji wana uelewa wakutosha juu ya CHF iliyoboreshwa ili wasipokee upotoshaji juu ya mabadiliko ya gharama za uchangiaji.

Pia maofisa maendeleo ya jamii wahamasishe wananchi vya kutosha na tutashindanisha wilaya na wilaya kila baada ya miezi mitatu” alisema. Dk Mahenge pia aliagiza Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri kusimamia kwa umakini shughuli za uandikishaji ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kila mwanachama wa CHF taarifa zake binafsi zimewekwa kwenye mtandao, makusanyo ya fedha yanaingizwa na yanafanywa kwa njia ya kielektroniki.

“Pia fedha za wanachama ziingizwe katika akaunti ya CHF Mkoa kwa wakati na taarifa za CHF na stakabadhi za kuwekea fedha benki ziwasilishwe kwa Katibu Tawala Mkoa mwisho wa mwezi,”alisema. Dk Mahenge aliwataka wakurugenzi hao kufuatilia utoaji huduma kwa wanachama na kama kuna changamoto wazitafutie ufumbuzi mapema ili zisiharibu taswira nzima ya mfumo wa CHF katika mkoa.

“Hii ni kazi yetu viongozi kufuatilia, ni muhimu, ...unakuta wakati mwingine hoja zinakwenda kwa viongozi wa juu kumbe zingeweza kutatuliwa katika gazi ya Kijiji au Wilaya…kasimamieni kuhakikisha CHF inakuwa agenda ya kudumu katika vikao vyote vya vijiji, au kata, wilaya hadi mkoa,” alisema.

Dkt. Mahenge aliwaagiza Wakurugenzi watendaji hao kuhakikisha kupitia bajeti za halmashauri wanatenga fedha kwa ajili ya kuhuisha kaya za wazee na kuendelea kuchangia wazee ambao hawana kadi za CHF hadi sasa na kuhakikisha vifaa kwa ajili ya huduma ya usajili wa wanachama vinanunuliwa kwa wakati.

Aliwataka Waganga wakuu wa wilaya kuhakikisha vituo vya kutolea huduma vinatumia fedha za dawa, vifaa na vifaa tiba na vitendanishi zinazoletwa kila mwezi kwa mujibu wa taratibu na miongozo iliyopo. Awali, Mbunge wa Mpwapwa, Mheshimiwa George Lubeleje alisema haipendezi kwa wanachama wa CHF kufika kwenye vituo vya afya na kutakiwa kwenda kununua dawa kutokana na vituo vya afya kukosa dawa.

Chanzo: habarileo.co.tz

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.