• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC 'avalia njuga' vitambulisho vya wajasiriamali

Imewekwa tarehe: May 22nd, 2019

SERIKALI ya Mkoa wa Dodoma imewataka wafanyabiashara wadogo wote kuwa na vitambulisho vya wajasiriamali vilivyotolewa na Mhe. Rais ili waweze kufanya biashara zao bila usumbufu wowote.

Agizo hilo limetolewa na  Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge alipokuwa akiongea na wafanyabiashara wadogo katika soko la Bonanza lililopo Kata ya Chamwino jana.

Dkt. Mahenge alisema kuwa, dhamira ya Rais Mhe. Dkt. John Magufuli ni kuwawezesha wafanyabiashara wadogo kufanya biashara zao pasipokuwa na usumbufu wa tozo mbalimbali.

“Maelekezo yangu ni kwamba kuanzia kesho Mei 22, 2019 muwe na vitambulisho vya wajasiriamali vilivyotolewa na Mhe. Rais kwa faida yenu…kigezo cha kuwa na kitambulisho ni mtaji wako, siyo meza unayofanyia biashara, mtaji ndiyo unaokutambulisha kuwa wewe ni wa kitambusho cha shilingi 20,000 au wewe ni wa Mamlaka ya Mapato Tanzania…haitaruhusiwa mtu kufanya biashara bila kitambulisho na ukivaa kitambulisho hakuna mtu kukudai ushuru” alisisitiza Dkt. Mahenge.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa, kwa wafanyabiashara ambao mtaji wao unazidi shilingi milioni nne, wao wanatakiwa kusajiliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania ili kulipa kodi ya Serikali.

“Kwa wafanyabiashara ambao mtaji wao hauzidi shilingi milioni nne, Mheshimiwa Rais amesema mtalipa shilingi 20,000 kwa mwaka mzima na kupewa kitambulisho” alisisitiza Dkt. Mahenge.

Aidha, aliwataka wafanyabiashara wadogo kufuata taratibu na sheria zilizopo katika kutekeleza majukumu yao ikiwemo kufanya usafi katika masoko, na kuepuka kupanga biashara zao kwenye maeneo yasiyoruhusiwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi alisema “maekelezo ya Mkuu wa Mkoa ni maelekezo halali…lengo la Mheshimiwa Rais ni kuwatumikia wananchi wanyonge ili wakuze mitaji yao na kuwa wafanyabiashara wakubwa” alisema Kunambi.

Alisema Halmashauri inatakiwa kufikiri tofauti, kuwa na mapato ya ndani ya kudumu.

“Haiingii akilini kufikiri kwamba Halmashauri ya Jiji kama letu  itegemee ‘petty collection’ kujiendesha” aliongeza Kunambi.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma alitembelea masoko ya Bonanza-Chamwino na Chang’ombe kuongea na wafanyabiashara wadogo akiambatana na Katibu Tawala Mkoa Maduka Kessy, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Patrobas Katambi  na Kamati za Ulinzi na Usalama za Mkoa na Wilaya.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.