• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC Dodoma azindua kampeni uhamasishaji wa CHF iliyoboreshwa

Imewekwa tarehe: May 22nd, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge amewahimiza wananchi wa Dodoma kujiunga na Mfuko wa Bima ya Afya ya Jamii (CHF iliyoboreshwa) ili iwasaidie kupata huduma bora za matibabu kwa gharama nafuu.

Dkt. Mahenge aliyasema hayo wiki iliyopita (14 Mei, 2020) alipokuwa akizindua kampeni ya uhamasishaji wananchi wa mkoa wa Dodoma, kampeni itakayotumia njia mbalimbali kuwafikia wananchi ikiwemo kupitia vyombo vya habari.

CHF iliyoboreshwa kwa sasa inatekelezwa nchi nzima na hivyo wananchi wanachangia kiwango kimoja ambacho ni shilingi 30,000/= (elfu thelathini) tu kwa kaya yenye watu 6 kwa mwaka mzima. Hii ni sawa na kila mtu kuchangia shilingi 5,000/= kwa mwaka.

Alielezea zaidi Dkt. Mahenge ametanabaisha kuwa taarifa ya maendeleo ya Mfuko wa CHF kwa kipindi  kilichoishia Juni, 2019 mkoa wa Dodoma ulisajili jumla ya kaya 17,366.  Kuanzia mwezi wa Julai, 2019 hadi Aprili ,2020 hali ipo kama ifuatavyo:

  • Jumla ya kaya 47,141 zimeshaandikishwa hadi kufikia tarehe 30 Aprili, 2020 na hadi sasa kuna kaya hai 30,758 (6.8%). Hii inamaana kuwa jumla ya kaya 16,383 hazijahuisha uanachama wao na hawawezi kupata matibabu kwa kutumia kadi za CHF.
  • Idadi hii ya kata zilizojiunga zina jumla ya wanufaika wapatao 282,846 na miongoni mwao wameweza kutumia kadi za CHF kupata huduma za matibabu kwa gharama nafuu kuanzia hatua ya Zahanati hadi Hospitali ya mkoa. Huduma hizo zimejumuisha upasuaji mdogo na mkubwa.
  • Kwa kipindi cha Julai 2019 hadi Aprili 2020 CHF imelipa zaidi ya vituo vya huduma 330 vilivyotibu wanachama ambapo jumla ya shilingi 496,821,324.94 zimelipwa baada ya kuwasilisha madai.
  • Aidha, Dkt. Mahenge ametoa maagizo kuwa katika kipindi cha mavuno mwezi Mei hadi Agosti, 2020 yafuatayo yanatakiwa kutekelezwa.
  • Kila Mkuu wa Wilaya na Wakurugenzi wafanya uhamasishaji wa jamii kujiunga na CHF katika Mitaa/Vitongoji na vijiji vyote, kila kijiji kisajili kaya zote ambazo hazijajiunga na Mfuko wa CHF.
  • Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wahakikishe kaya zote (16,383) ambazo hazijahuisha uanachama  zifikiwe, zihamasishwe ili walipe ada ya CHF kwa ajili ya gharama za matibabu.
  • Wakurugenzi wa Halmashauri wasimamie vizuri timu za CHF kutekeleza majukumu yao na  kuhakikisha michango ya wanachama wa CHF inawekwa kwenye akaunti ya mfuko wa afya Dodoma na taarifa zinawekwa kwenye mfumo wa CHF-IMIS.
  • Wakurugenzi na Maafisa Utumishi wa Halmashauri  wahakikishe Watendaji wa Vijiji na Mitaa wanatimiza wajibu wao kusimamia uhamasishaji na kuhakikisha kila kijiji kinaandikisha kaya zote ambazo hazijajiunga na Mfuko wa CHF.
  • Mganga Mkuu wa Mkoa na Waganga Wakuu wa Wilaya kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora kwa wanachama wa CHF ili waweze kutoa ushuhuda mzuri kwa wananchi ambao hawajajiunga na CHF. Aidha, wahakikishe vituo vya huduma wanawasilisha madai ya wateja waliotibiwa kwenye mfumo wa kielektroniki (CHF-IMIS) kwa wakati na kutumia fedha zinazolipwa kwenye vituo kulingana na mwongozo.
  • Timu ya CHF ya Mkoa kwa ushirikiano na Halmashauri  kuhakikisha wanaandaa mpango mkakati wa CHF wa Mkoa ili iwe rahisi kupima utekelezaji wa usajili wa CHF kwa kila Halmashauri.
  • Timu ya uratibu wa CHF ifanye zoezi la kutoa elimu ya faida za CHF na uhamasishaji wa wananchi kujiunga na mfuko kuwa endelevu na lijumuishe njia mbalimbali za upashanaji habari.

Akimalizia Mkuu wa Mkoa  alisema kuwa "ni imani yangu tukifanya kazi kwa ushirikiano katika kutekeleza mikakati hii tuliyojiwekea na maelekezo haya tuliyopeana katika kazi hii, tukiweza kufika vijijini/mitaa yote katika Mkoa wa Dodoma tutasajili kaya zote ambazo hazina kadi za CHF". Dkt. Mahenge alimalizia maelezo yake kwa kuzindua rasmi kampeni ya uhamasishaji jamii kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF iliyoboreshwa) kwa mwaka 2020.

Bofya hapa kusoma hotuba ya uzinduzi: HOTUBA YA UZINDUZI WA UHAMASISHAJI CHF 2020 RC DODOMA



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.