• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC Mahenge ahimiza mazingira rafiki kwa wawekezaji

Imewekwa tarehe: April 29th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dkt Binilith Mahenge amezitaka halmashauri zote za Mkoa wa Dodoma kuweka mazingira mazuri kwa ajili ya kupokea wawekezaji ili kuwavutia wawekezaji kuja kuwekeza katika Mkoa wa Dodoma hasa baada ya kuwa makao makuu na kuwa na fursa nyingi.

Dkt Mahenge ametoa maagizo hayo jijini Dodoma wakati wa kikao cha kamati ya ushauri cha Mkoa (RCC) ambapo amesema bado kuna changamoto katika maandalizi katika halmashauri nyingi pindi zinapopokea wawekezaji.

Amezitaka halmashauri zote kuweka mazingira mazuri hasa katika kuwapokea wawekezaji na namna ya kuwahendo wawekezaji pindi wanapoingia katika maeneo yao kwa lengo la kutaka kuwekeza maeneo hayo.

“Nataka maeneo yote yawe tayari kwa ajili ya uwekezaji muwekezaji anapokuja anataka huduma zote za muhimu ziwepo katika eneo husika, sio muwekezaji anakuja unaambiwa ukianza ujenzi ndio tunakuletea huduma za maji, umeme na barabara” amesema Dkt Mahenge.

Aidha amewataka viongozi wa ngazi zote katika halmashauri kuweka mkazo katika kusimamia miradi ya maendeleo hasa miradi ya maji ambapo tatizo limekuwa sugu katika maeneo mbalimbali kwa usimamizi hafifu kutoka kwa viongozi.

“Katika maeneo mengi miradi hasa ya maji haikamiliki kwa wakati, hii sio miradi ya RUWASA peke yao hii ni miradi ya wananchi katika maeneo yetu, unakuta miradi haikamiliki na viongozi kwenye kata wapo” amesema.

Pia amesisitiza usimamizi madhubuti wa fedha za asilimia kumi (10) zinazotelewa na halmashauri kwa makundi ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu, kwa kusema fedha hizo hazisimamiwi kikamilifu na kupelekea kuto kuwa na tija katika makundi hayo.

“Kuna kikundi kimoja cha wanawake wamepewa mkopo na kununua ng’ombe lakini mtu aliyewaletea ng’ombe hao ameleta ng’ombe hajapandishwa tena kamtoa mbali, shida mtu aliyepewa kazi hiyo hana utaalamu wowote na kuwapa mzigo kumuhudumia ng’ombe huyo” amesema.

Amebainisha kuwa ofisi yake imeandaa kitabu maalumu kinachoonyesha utekelezaji wa miradi na shughuli zote zilizofanywa na Mkoa wa Dodoma kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita kikijumuisha makongamano waliyoyafanya kama Mkoa.

Pia Dkt Mahenge amewataka viongozi kwenda kuyasimamia yote waliyokubaliana kupitia kikao hicho ili wanapokutana katika vikao vingine mambo mengi yawe yametekelezeka kikamilifu ili kufikia malengo ya serikali katika kuwahudumia wananchi.

Awali Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Maduka Kessy amewaonya wale wote wenye tabia ya kufuja mapato kwa kukusanya mapato nje ya mfumo kwa lengo la kufuja mapato hayo kwa kuwa kwa uzoefu wake mifumo hiyo ipo sahihi lakini kuna baadhi ya watu wanafanya makusudi ili zionekane hazina ufanisi katika utendaji kazi.

Nae Mbunge wa jimbo la Kibakwe Wilayani Mpwapwa ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi Mheshimiwa George Simbachawene ameshauri halmashauri kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa ardhi katika maeneo yao hasa baada ya ujio wa makao makuu ili wananchi wanufaike na ardhi hiyo kwa halmashauri hizo kupima ardhi kuiongezea thamani.

“Ukiangalia maeneo mengi ardhi ipo tu na watu wengi wanakuja wananunua kama mashamba hii sio sawa wananchi wetu waelimishwe umuhimu wa ardhi na ardhi hiyo ipimwe” amesema Waziri Simbachawene.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.