• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC Mahenge akagua miradi, athari za mvua

Imewekwa tarehe: January 10th, 2020

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge ameipongeza  Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kutekeleza miradi ya kimkakati  inayolenga kutoa huduma kwa wananchi   ikiwemo ujenzi wa soko kuu linalojulikana kama soko la  Ndugai pamoja na miradi mingine ambapo amewakumbusha kuikamilisha kwa wakati.

Aliyasema hayo katika ziara yake jijini humo mapema leo asubuhi Januari 10, 2020 ambapo aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Patrobas Katambi na viongozi wengine wa Mkoa huo.

Mkuu huyo wa Mkoa alipewa taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo inayoendelea kujengwa katika hatua za mwisho katika Jiji la Dodoma ambayo ni ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi, soko kuu la Ndugai, uboreshaji wa bustani ya mapumziko katika eneo la Chinangali pamoja na kituo kikuu cha kuegesha malori eneo la Nala.

“Niwapongeze kwa hatua mliyofikia, mmepiga hatua katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati, kwa hatua miradi hii ilipofikia nina imani tarehe mliyoahidi kuikamilisha mtakuwa tayari, Februari 15 siyo mbali hakikisheni inakuwa kama mlivyoahidi,” alisema Dkt. Mahenge.

Awali wakati wa ziara hiyo, pia Dkt. Mahenge alitembelea mtaa wa Nyakongo Kata ya Nkuhungu kukagua athari za mvua, ambapo eneo hilo limekumbwa na mafuriko kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha Jijini humo.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, mwenyekiti wa mtaa huo  Matonya Chiwaligo alisema kuwa  eneo hilo halina miundombinu ya kutiririsha maji  ya mvua hali inayopelekea kuishia kwenye makazi ya watu.

Kufuatia hali hiyo, mkuu huyo wa mkoa ameziagiza mamlaka zinazohusika na miundombinu ya maji wakiwemo wakala wa barabara za mjini  na vijijini (TARURA) na wakala wa barabara (TANROADS) kukutana haraka na kuweka mpango wa pamoja katika kulinusuru eneo hilo na mafuriko.

“Nawaagiza wote wanaohusika na hili, hakikisheni mnakutana  mara moja ili mlipatie ufumbuzi wa haraka eneo hili, TARURA na TANROADS kupitia wataalamu wenu shirikianeni katika kulitatua hili kwa wakati kabla ya januari 30, 2020 eneo hili liwe limewekwa miundombinu ya kutiririsha maji,” alisisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Aidha, amewaagiza viongozi wote wa Mkoa wa Dodoma kuhakikisha wanakuwa na utaratibu wa kutunza taarifa za kazi na changamoto wanazozitatua kwa wananchi na kuonyesha zilizotatuliwa na zilizopelekwa katika ngazi za juu za maamuzi ili  kuboresha huduma kwa wananchi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.