• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC Mahenge afika Mtera kukagua utekelezaji agizo la Rais

Imewekwa tarehe: October 14th, 2020

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dkt.  Binilith Mahenge amemuagiza Mhandisi wa Maji (RUWASA) Wilaya ya Mpwapwa katika eneo la Mtera kukarabati kwa wakati miundombinu ya upelekaji maji kutoka katika bwawa la Mtera kwenda kwa wananchi wanaoishi katika maeneo ya jirani.

Dkt. Mahenge alisema hayo katika ziara yake ya kutembelea na kukagua ukarabati miundombinu ya maji ambayo inatoka katika bwawa la Mtera na kwenda kwa wananchi.

Aidha, Mahenge amesisitiza kuwa wananchi wanauhitaji mkubwa wa maji na Mheshimiwa Rais ameshatoa maagizo tangu awali wananchi waweze kupata huduma ya maji katika bwawa hilo lakini pia matarijio ya mji kuwa mkubwa hapo baadae ni makubwa mno katika eneo hilo la Mtera.

"Nimembelea na kukagua miundombinu yote, ninachokiona kinaweza kurahisisha sisi kutekeleza agizo la Mheshimiwa Rais, wananchi kupata maji kwa uhakika kutoka katika bwawa hili la Mtera. Kwa maana hiyo kwa awamu hii ya kwanza mnahitajika kurekebisha mashine hizi za mwanzo mbili na kuongeza ukubwa wa kipenyo cha bomba kinacho toa maji kwa wananchi wakati tukiendelea kusanifu mradi wa muda mrefu kwani tuna matajarajio ya mji huu kuja kuwa mkubwa na mahitaji ya maji yataongezeka” alisema Dkt. Mahenge.

Vile vile, kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Mhe. Jabir Shekimweri amesema kuwa wamepokea maelekezo yote kutoka kwa mkuu huyo na watayatekeleza kama alivyokwisha kuelekeza hapo awali wakiwa wanafanya ukaguzi katika miundombinu hio. "Tunakushukuru Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa kwa ziara yako ya ukaguzi wa utekelezaji wa agizo la Mheshimiwa Rais kuwa wananchi wa maeneo haya ya Mtera waweze kupata maji. Maelekezo yako tumeyachukua na tutayafanyia kazi ipasavyo ilituweze kufanikisha mradi huu kwa awamu ya kwanza huku tukiendelea kusanifu mradi mkubwa na wa muda mrefu kutokana na matarajio yetu ya eneo hili la Mtera kuwa na ongezeko la uhitaji wa maji’’ alisema Mhe. Shekimweri.

Hata hivyo, Mhandisi wa Maji (RUWASA) Mkoa wa Dodoma, Godfrey Mbabaye ametoa tathmini ya utekelezaji wa mradi huo mkubwa utakaokidhi ongezeko la mahitaji ya watu ambapo mradi huo utaghalimu shilingi Bilioni 1.6 na kwa hatua za awali wameishaanza usanifu.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge (wa kwanza kulia) akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri (wa kwanza kushoto) alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa agizo la Rais kuhusu maji kuwafikia wananchi wa jirani na Bwawa la Mtera.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.