• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC Mahenge ataka tathimini vifo vya mama na mtoto

Imewekwa tarehe: February 23rd, 2021

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dkt Binilith Mahenge ametaka kufanyika kwa tathmini juu ya sera na matamko yanayohusu udhibiti wa vifo vya mama na mtoto yanayotolewa kama yanasaidia katika udhibiti wa vifo vya uzazi hapa nchini.

Dkt Mahenge ametoa ushauri huo jijini Dodoma wakati akifungua kikao kazi cha kujadili mpango mkakati wa kupunguza vifo vya mama na mtoto kinachofanyika Dodoma baina ya wakurugenzi wa Halmashauri, waganga wa hospital na wadau wa sekta ya afya kanda ya kati.

Amesema mara nyingi kumekuwa na matamko mengi na sera juu ya udhibiti wa vifo vya mama na mtoto imefika wakati kufanyatathmini kuona ufanisi wa sera na matamko hayo.

“Tuna matamko mengi na sera je zimetufikisha wapi, nashauri mkae muangalie tumefanikiwa wapi na tumekwama wapi ili turekebishe kupunguza hivi vifo vya mama na mtoto ambavyo vingi vinaepukika” amesema Dkt Mahenge.

Amesema takwimu zinaonyesha vifo vya uzazi vinaongezeka ambapo kwa mwaka 2018 hadi 2020 vimekuwa vikiongezeka licha ya mikakati iliyofanyika kwa kanda ya kati 2019 kulikuwa na vifo 162 na mwaka 2020 ilikuwa 175.

Amesema miongoni mwa vitu vinavyochangia vifo hivyo ni kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua kwa akina mama, kifafa cha mimba, kupasuka kwa mji wa uzazi na uambukizo mkali, ambavyo vinaweza kuzuilika na kupunguza vifo vya uzazi.

Ameongeza kuwa “vifo vya watoto wachanga pia ni changamoto katika kanda hii takwimu zinaonyesha kupungua kwa mwaka 2019 vifo 1,173 na mwaka 2020 kulikuwa na vifo 1,009” amesema.

Ametaja vitu vinavyosababisha vifo kwa watoto ni kushindwa kupumua baada ya kuzaliwa, mtoto kuzaliwa kabla ya wakati na mtoto kuzaliwa na uzito pungufu na neumoni.

Amewataka wakurugenzi kuhakikisha watoto wanaotakiwa kwenda shule wanakwenda ili angalau wapate elimu ambayo itasaidia kuwa na uelewa katika jamii hali itakayopunguza vifo vya uzazi kwa jamii kuwa na elimu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa huduma ya kinga kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia wazee na watoto Dkt Leonard Subi amesema mpaka sasa wamepiga hatua kubwa katika mapambano kuzuia vifo vya mama na mtoto kwa kuimarisha huduma za Msingi na Sekondari.

Amesema katika kikao hicho watatumia katika kutathmini utekelezaji wa mpango wa mapambano dhidi ya kupunguza vifo vya uzazi hasa kwa mama na mtoto na kuweka mikakati mipya kuhakikisha wanapunguza vifo vya uzazi na kupokea utekelezaji wa mpango huo kwa halmashauri.

Amesema kwa sasa wameimarisha sana miondombinu kama hospitali, vituo vya Afya na zahanati kuhakikisha huduma hizo zinafikiwa na wananchi kwa wakati na kwa urahisi sana kupunguza vifo vya mama na mtoto ikiwa na ushirikishwaji katika ngazi mbalimbali hadi ngazi ya kaya.

Amesema kama Wizara wanafanya kila jitihada kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vifo vya uzazi vipungue kwa kiasi kikubwa hadi kufika vifo chini ya 70 kati ya vizazi laki moja (100,000) katika kuhakikisha tatizo hilo linapungua na kuwa na takwimu sahihi amewataka wakurugenzi kupata takwimu za vifo vya uzazi kila siku asubuhi wakishirikiana na watendaji wa ngazi zote katika halmashauri zao.

“Nikiuliza hapa kila Mkurugenzi takwimu za vifo katika halmashauri yake hana jibu mpaka aulize kwa wataalamu wake kuanzia sasa nataka takwimu hizo mzipate kila siku” amesema Dkt Subi.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.