• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC Mtaka aagiza kila kaya Dodoma ipande miti

Imewekwa tarehe: September 28th, 2021

Na Binde Constantine, DODOMA.

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Antony Mtaka ametoa agizo kwa wananchi wa kaya zote za Dodoma, wanaomiliki viwanja na tayari wana umiliki wa hatimiliki ya viwanja hivyo, kuhakikisha wanapanda miti katika maeneo yao, ikiwa ni utekelezaji wa kampeni ya kimkoa ya kuhakikisha kwamba kila kaya au kiwanja kinapandwa miti.

Mtaka aliyasema hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya Ismaili Civic yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya Sekondari ya Bunge Septemba 26, 2021 ambapo Ismaili Civic walitoa miti 1,000 iliyopandwa katika shule hiyo, zoezi lililoongozwa na Mkuu huyo wa Mkoa.

“Sisi kama Mkoa tupo kwenye kampeni ya kuhakikisha kwamba kila kaya wanapanda miti, na changamoto kubwa ya watu wa Dodoma ni upandaji wa miti, kwa hiyo maudhui ya mwaka huu kwa mkoa wa Dodoma ni kuhakikisha wananchi wa Dodoma wanajitahidi kupanda miti” alisema Mtaka.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa huo, Dkt. Fatma Mganga, alitoa wito kwa wanafunzi wa shule hiyo waitunze na kuisamamia miti hiyo ili iweze kukua na kustawi vizuri kwa lengo la kupendezesha mazingira ya shule hiyo mpya huku akiahidi kufuatilia maendeleo ya miti iliyopandwa.

“Mkuu wa shule ukishirikina na walimu pamoja na wanafunzi, naagiza muitunze miti hii iliyopandwa leo lakini na mimi nitakua nanyi bega kwa bega kutunza hii miti ili mwisho wa siku tuweze kuona matunda yake” alisema Mganga.    

Aidha, Makamu wa Rais wa Jumuiya ya Ismaili Civic, Nazir Thawer alitoa wito kwa wananchi wa Dodoma kutunza mazingira ikiambatana na upandaji wa miti katika maeneo yanayowazunguka ikizingatiwa kuwa maudhui yao ya mwaka huu wa 2021 ni usimamizi na utunzaji wa mazingira.

“Katika ufanyaji wa kazi za kijamii tumejitolea wafanyakazi takribani 20,000 kidunia, wakifanya kazi kwa masaa laki moja ya kutoa huduma, mwaka huu maudhui yetu ni usimamizi na utunzaji wa mazingira, ambao utahusisha ukarabati na usafi katika maeneo ya Umma ili kuweka hali nzuri na endelevu katika maeneo yetu” alisema Nazir.

Akitoa shukrani, Mkuu wa Shule ya Sekondari Bunge, Salome Elias aliishukuru ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Jumuiya ya Ismaili Civic kwa kuichagua shule hiyo kuipa msaada wa miti hiyo kwani itasaidia katika kutengeneza mazingira rafiki ya kujisomea kwa wanafunzi wake na aliahidi kutunza miti hiyo.

“Sisi kwetu ni baraka kwa sababu tuna changamoto ya upepo kwahiyo tukiona watu wanatusaidia tunaona dalili za mabadiliko, nitumie fursa hii kuahidi watu wote mliopo hapa leo na kwako Mkuu wa Mkoa kwamba hii miti tutaitunza” alisema Mkuu huyo wa shule.






Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.