• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC Mtaka akutana na wafanyabiashara wakubwa

Imewekwa tarehe: June 21st, 2021

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka amekutana na kufanya mazungumzo na Wafanyabiashara wakubwa Mkoani Dodoma kwa lengo la kupokea maoni yao kuhusu Mazingira ya ufanyaji biashara na uwekezaji katika Mkoa wa Dodoma.

Kikao hicho kilichofanyika kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, kimewajumuisha Wafanyabiashara wakubwa kutoka sekta mbalimbali, wakuu wa Taasisi zinazotoa huduma na zinazosimamia masuala ya biashara na uwekezaji zikiwemo Idara ya Kazi, Wakala wa Vipimo, TANESCO, TARURA, DUWASA, TIC, TRA, TBS, OSHA, TMDA na Viongozi wa Halmashauri ya jiji la Dodoma.

Mtaka amewaeleza wafanyabiashara kuwa yeye ni muumini Mkubwa wa Sekta Binafsi kwa kutambua ukweli kuwa ndio wachavushaji wa uchumi kukua na kwamba licha ya Serikali kuwa Muajiri Mkuu, Sekta Binafsi imeendelea kuwa muajiri wa wakati wote huku ikiwa na fursa lukuki za kufanya uchumi na uzalishaji.

“Tukitaka jiji la Dodoma liwe shindani ndani na nje ya jumuiya ya Afrika Mashariki, liweze kushindana na majiji kama Nairobi, Kampala, Bujumbura, Kigali na Majiji mengine makubwa nje ya Afrika, lazima Sekta Binafsi ijipambanue na kustawisha shughuli zake na katika kipindi cha uongozi wangu kama Mkuu wa Mkoa wa Dodoma nitahakikisha Serikali inailinda Sekta Binafsi” alibainisha Mhe. Mtaka.

Aliwataka Wadau wa Sekta Binafsi katika Mkoa wa Dodoma kujipanga vema ili kuweza kufaidika na fursa za kuwekeza zinazotokana na Serikali kuhamishia shughuli zake Makao Makuu ya Nchi na hata wanapokuja Wawekezaji wakubwa kutoka Nje ya Nchi, Sekta Binafsi waweze kuingia nao mashirikiano katika uwekezaji mbalimbali.

Nae Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara, Wakulima na Wenye Viwanda Mkoa wa Dodoma – TCCIA Ndg. Deus Nyabiri ameitaka serikali kupitia Mamlaka ya Mapato TRA kuhakikisha inaongeza program za utoaji elimu ya kodi na kuhakikisha inawafikia Wafanyabiashara wote kuanzia Wakubwa hadi wajasiriamali wadogo ili wawe na utamaduni wa kulipa kodi wao wenmyewe bila kushurutishwa.

Aidha, ameitaka Halmashauri ya Jiji la Dodoma kushindana na majiji mengine makubwa ndani na nje ya Afrika kwa kuboresha miundombinu ya maeneo ya kufanyia biashara kama vile masoko, vituo vya mabasi na kuweka mifumo rafiki ya uendeshaji ambayo haitageuka kero kwa wananchi wanaotegemea huduma hizo.

Ametoa Rai kwa Uongozi wa Mkoa wa Dodoma kuhakikisha inahuisha mabaraza ya biashara ya Mkoa na Wilaya na Majukwaa ya Kodi ili yafanye kazi yake ya msingi ya kuwa majukwaa ya majadiliano kati ya wafanyabiashara/wawekezaji na serikali na taasisi zake ili kuendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji katika Mkoa wa Dodoma.

Kwa upande wake Mjumbe wa TCCIA Taifa Ndg. Faustine Mwakalinga amezitaka Taasisi mbalimbali za Serikali zinazosimamia shughuli za biashara na uwekezaji kufanya kazi kwa ushirikiano kama timu mmoja ili kuondoa urasimu, usumbufu na ucheleweshaji wa utekelezaji miradi kwa kuchelewesha au kukwamisha vibali mbalimbali.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.