• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC Mtaka aridhishwa ujenzi madarasa

Imewekwa tarehe: December 23rd, 2021

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Antony Mtaka, ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa yanayojengwa kupitia fedha za mapambano dhidi ya UVIKO- 19 ambapo Mkoa huo unatarajia kukabidhi madarasa 601 Disemba 30 mwaka huu.

Hayo ameyasema leo Disemba 22, 2021 jijini Dodoma mara baada ya kufanya ziara pamoja na Kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Dodoma ya kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule za sekondari.

Mtaka amesema kuwa ujenzi wa madarasa unakwenda vizuri na matarajio ya mkoa ni  kukabidhi vyumba vyote vya madarasa ifikapo Disemba 30 mwaka huu. “Kama mkoa tumeridhika na hatua ya ujenzi ilipofikia na tunataraji kufanya hafla ya kukabidi vyumba hivi 601 vya mkoa katika wilaya mojawapo ambayo tutaichagua kwa niaba ya mkoa” amesema Mkuu huyo wa Mkoa.

Aidha Mtaka ameziagiza wilaya zote ambazo zinatekeleza mradi huo wa ujenzi wa vyumba vya madarasa kuhakikisha kuwa zinapanda miti katika maeneo ya shule. “Wakati madarasa haya yanajengwa naomba yaendane na zoezi la upandaji wa miti, haiwezakani shule inakuwa na majengo mazuri lakini maeneo yake yamepauka lazima kila mwanafunzi apate mti mmoja wa kuutunza” amesema Mtaka.

Hata hivyo Mtaka amewataka wazazi na walezi ambao watoto wao wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kuhakikisha ifikapo Januari 17 Mwaka 2022 watoto wote wawepo shuleni. “Itakuwa ni aibu kubwa kuwa na majengo mazuri na ya kisasa ambayo yanajitosheleza lakini watoto hawaendi shule, hatutaki kuona watoto wanaonekana sokoni, mitaani pamoja na mashambani au kuwa sehemu ya kutunza familia” amesisitiza Mtaka.

Pia ameutaka uongozi wa Jiji la Dodoma kuhakikisha unakamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa wakati ili watoto wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza waweze kusoma.

Kwa upande wake Katibu Tawala mkoa wa Dodoma Dk. Fatma Mganga, amesema kuwa ujenzi wa vyumba vya madarasa 601 unagharimu kiasi cha Sh. bilioni 12.02 kwa shule za sekondari, lakini pia mkoa wa Dodoma unajenga madarasa 175 kwa ajili ya shule shikizi ambayo yataghalimu kiasi cha Sh.bilioni 3.5.

Awali Mkurugenzi wa jiji la Dodoma Joseph Mafuru ameihakikishia Kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Dodoma kuwa hadi ifikapo Disemba 24 mwaka huu madarasa hayo yatakuwa tayari. “Sisi kama Jiji tunajitahidi katika kutekeleza mradi huu na tunamshukuru sana mheshimiwa Rais kuona umuhimu wa watoto ambao walikuwa wanakosa nafasi kuweza kusoma" alisema Mafuru.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka akimuangalia mmoja wa mafundi wa 'tiles' akiendelea na kazi wakazi wa ziara yake ya ukaguzi wa maendeleo ya kazi za ujenzi wa madarasa.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mkata akikagua ujenzi wa madarasa akiwa ameambatana pia na maafisa kutoka Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru akiongea kuhusu utekelezaji wa shughuli za ujenzi wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Anthony Mtaka.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.