• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC Mtaka awapa angalizo Wakuu wa Wilaya Dodoma

Imewekwa tarehe: June 22nd, 2021

Na Noelina Kimolo, DODOMA.

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Antony Mtaka   amewataka Wakuu wa Wilaya za Mkoa huo kutambua kuwa wao ni wawakilishi wa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Wilaya zao hivyo wafanye kazi huku wakitambua dhamana waliyoibeba.

Kauli hiyo ameitoa wakati wa hafla fupi ya uapisho wa Wakuu wa Wilaya wapya wa Kongwa na Kondoa iliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya Mkuu wa Mkoa mapema leo Juni 22, 2021.

Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka Wakuu hao wa Wilaya wawe na ushirikiano wa kutosha na viongozi mbalimbali katika wilaya, ili kuendeleza kasi ya  maendeleo makubwa kwenye mkoa huo ambao ni Makao Makuu ya Nchi.

“Tengeneza hadidhi yako kwa kuleta maendeleo katika sehemu ambayo unakuwepo, hata ukiondoka watu waone kitu ambacho umekifanya” alisema Mtaka.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kondoa Khamis Mkanachi, alisema kutokana na imani ya Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan kwake, atahakikisha  kuwa anafanya kazi kwa juhudi kwa kushirikiana na viongozi wenzake pamoja na wananchi wa Wilaya ya Kondoa kwa ujumla.

“Kuanzisha kilimo cha kisasa, elimu, afya na sekta binafsi ni vitu ambavyo  wewe Mkuu wa Mkoa uliahidi kuvipa kipaumbele, tunaambatana na wewe kwa hayo uliyoyaonesha kama dira na sisi tutayasimamia haya kwa kiwango cha juu” alisema Mkanachi.

Aidha, alisema kuwa wao ni watumishi na siyo watawala, wanakwenda kuhudumia jamii na wanatamani kuonesha utofauti kwa huduma watakayotoa katika jamiii ili imani walizopewa zikaonekane.

Naye  mkuu wa Wilaya ya Kongwa Remedius Emmanuel, alisema anahitaji sana ushirikiano kutoka kwa Wakuu wa Wilaya wengine, viongozi pamoja na wananchi wote wa Mkoa wa Dodoma katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku.

“Kazi yangu ni kutekeleza ile imani ambayo Mhe. Rais ameionesha kwangu kama kijana, na hivi karibuni alisema atachagua vijana, sasa mimi ni miongoni mwa hao vijana hivyo kazi yangu ni kuendelea kuleta mchango wa vijana katika Taifa letu” alisema Emmanuel.

Wakuu hao wa Wilaya waliteuliwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hivi karibuni ambapo kwa mujibu wa taratibu wataapishwa na Wakuu wa Mikoa husika.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma atoa pongezi kwa Madiwani

    May 25, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Wananchi Kata ya Madukani washukuru kuboreshwa huduma za Afya, Zahanati ya Chikande

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.