• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC Senyamule aja na mbinu kuinua elimu Dodoma

Imewekwa tarehe: September 8th, 2022

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule amewataka Wakuu wa Shule za Mkoa huo kuanzia ngazi ya Elimu msingi na Sekondari kuhakikisha wanatoa ripoti ya utoro na maendeleo ya wanafunzi kila ifikapo Ijumaa ya kila wiki kuanzia ngazi ya kata mpaka mkoa ili kudhibiti utoro kwa wanafunzi.

Hayo ameyasema wakati akifungua kikao kazi cha kukabidhi mkakati wa kuimarisha ujifunzaji na ufundishaji ngazi ya elimu msingi na sekondari kwa Maafisa elimu,Wakuu wa Shule za Mkoa wa Dodoma pamoja na wadau wa elimu jumatano katikati ya wiki hii ya Septemba tarehe 07,2022.

Aidha Senyamule amewataka maafisa elimu na wakuu hao wa shule kuwa wabunifu katika kutatua changamoto mbalimbali zinazozikabili shule za mkoa wa Dodoma na wao kutokuwa chanzo cha changamoto hizo.

"Msiwe sehemu ya matatizo kazi kubwa mliyopewa ni kutatua matatizo hasa nyie maafisa elimu ambapo Mkuu wa shule anakuletea changamoto badala ya kutatua wewe unakuwa sehemu ya hiyo changamoto niwaombe tatueni changamoto pindi zinapowafikia," Amesema Senyamule.

Pia Mhe. Senyamule amewataka Maafisa Elimu kutokaa Ofisini muda wote wakati kuna shule nyingi za kutembelea na kubaini changamoto zilizopo na kuzitatua na sio kutumia muda mwingi kuandika taarifa wakiwa ofisini.

Kwa upande wake Katibu tawala wa Mkoa wa Dodoma Dkt.Fatuma Mganga amesema kuwa ameona ipo haja ya kubadili gia katika sekta ya elimu kutokana na matokeo ya Moku Mkoa wa Dodoma kutoridhisha.

"Bila kuchukua maamuzi magumu katika sekta hii nyeti ya elimu tutaendelea kuona viwango vyetu kama mkoa zinazidi kushuka siku hadi siku ni vyema tukachukua hatua za haraka kiukweli hatupo nafasi nzuri kabisa na mjue tu sisi ni jicho kila mmoja anatuangalia sisi tu, " Amesema Mganga.

Nae Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru amesema kuwa hawatakuwa tayari kuendelea kukaa na watendaji ambao hawatekelezi majukumu yao vizuri kuendana na kasi inayohitajika hivyo watapeleka mapendekezo kwenye ofisi ya katibu tawala ili kwa wale ambao wameonakana hawatendi kazi kisawasawa kwani ndio wanaosababisha tuendelee kuwa nyuma.

"Siku sio nyingi tutaanza kuwaondoa watendaji ambao wanatukwamisha kufikia malengo yetu nitahakikisha naleta majina ya watendaji wa ngazi yeyote ile wanaotukwamisha maana kuna watumishi wanatamani sana kufanya kazi hapa ila waliopo hapa wanaendelea kuchezea nafasi hizo ukweli tutaondoana ili kila mmoja alinde nafasi yake" Amesema Mafuru.

Kikao kazi hicho cha wadau wa elimu mkoa wa Dodoma kimekaliwa ili kuleta mawazo yatakayosaidia kuleta mageuzi ya elimu itakayoendana na hadhi ya makao makuu nchi.

DODOMA FAHARI YA WATANZANIA



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.