• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

RC. Senyamule atoa wito kwa shule zote za Dodoma kutafuta maeneo kwa ajili ya michezo

Imewekwa tarehe: March 21st, 2024

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule ametoa wito kwa shule zote zilizopo Mkoani Dodoma kuhakikisha zinatafuta maeneo kwaajili ya michezo kwa wanafunzi kwasababu michezo inajenga  afya ya akili na mwili.

Wito huo aliutoa katika hafla ya uzinduzi wa wiki ya wadau wa elimu kwa Mkoa wa Dodoma pamoja na ugawaji wa mipira 1000 kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kwa Halmashauri zote zilizopo Dodoma lengo likiwa kuwasaidia wanafunzi kuendelea kujifunza michezo kwa ufanisi.

“Nimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuunga mkono sekta ya michezo kwa kuhakikisha Tanzania inajiandaa kushindana katika mashindano makubwa duniani, pia kwa kuwaandaa vijana kwaajili ya kuitumikia timu ya Taifa na kufanya vizuri katika sekta ya michezo duniani. Nitoe shukrani kwa uongozi wa TFF kwa kutuwezesha mipira ambayo itatumika katika kuinua vipaji kwa wanafunzi katika mkoa wa Dodoma” alisema Senyamule.

Alisema shule zote zitakazopata mipira zitafuatiliwa na kuhakikisha inatumika vyema na kuwakilisha vizuri Mkoa katika michezo ya UMISETA kwa kufanya mazoezi kila siku kwasababu mipira ni bora na imara hivyo, isifungiwe bali itumike vyema.

Kwa upande wake Mwalimu Nestory Ngimbuzi, kutoka shule ya Msingi Fufu aliishukuru serikali kwa kutoa mipira ambayo itawasaidia watoto katika kuonesha vipaji vyao kwa sababu imekuwa ngumu kufuata ratiba ya michezo kutokana na ukosefu wa vifaa.

“Tunashukuru sana kwani imekuwa ni ndoto za wanafunzi wengi kukuza vipaji vyao. Michezo ni ajira hivyo, tunaamini mipira hii itakuwa chachu ya maendeleo ya sekta ya michezo kwa wanafunzi hapa Dodoma. Hapo mwanzo wanafunzi walikuwa wanatumia mipira ambayo wanatengeneza wenyewe kwa vitambaa na kamba kitu ambacho kilikuwa kinawafanya wasicheze kwa ufanisi” alisema Ngimbuzi.

Ikumbukwe kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya mageuzi katika sekta ya michezo ikiwemo kutoa hamasa kwa wachezaji wa timu ya Taifa na timu za Tanzania zinazoshiriki mashindano ya kimataifa pia ukarabati na ujenzi wa viwanja vipya vya michezo ikiwa ni katika harakati za kujiandaa na mashindano ya AFCON 2027.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.