• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Redio Jiji la Dodoma zatoa mchango mkubwa sekta ya elimu

Imewekwa tarehe: May 6th, 2020

Redio za ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma zimekuwa na mchango mkubwa katika kuwafundisha wanafunzi wa shule za msingi na sekondari katika kipindi hiki cha mapambano dhidi ya ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya corona.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa Elimu Sekondari wa Halmashari ya Jiji la Dodoma, Mwalimu Upendo Rweyemamu alipokuwa akihojiwa katika kipindi cha 'Dodoma Live' kinachorushwa na kituo cha redio Dodoma FM kupitia masafa ya 98.4 leo asubuhi.

Mwalimu Rweyemamu amesema kuwa katika kipindi cha mapumziko ya mapambano ya dhidi ya virusi vya corona baada ya shule kufungwa wanafunzi walikuwa wakizurura mitaani kwa kukosa kazi ya kufanya.

"Halmashauri ya Jiji la Dodoma iliona kuwa hilo ni tatizo kwa ukuaji wa sekta ya elimu na mapambano dhidi ya virusi vya corona. Halmashauri ikaamua kuja na mkakati wa kunusuru sekta hiyo kwa kubuni mpango wa kuwafundisha wanafunzi kupitia vipindi vya redio zilizopo ndani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma na mitandao ya kijami kama youtube. Katika kufanikisha dhamira hii, redio zimekuwa na mchango mkubwa sana. Nawapongeze redio Dodoma FM kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kukuza sekta ya elimu jijini Dodoma" alisema Mwalimu Rweyemamu.

Akijibu swali juu ya walengwa wa progamu hiyo, amesema kuwa imelenga wanafunzi wa kidato cha pili na kidato cha nne na wanafunzi wa darasa la nne na la saba ambayo ni madarasa ya mitihani.

Katika kuhakikisha elimu hiyo inawafikia na kuwanufaisha wananfuzi wengi, Afisa Elimu huyo amewataka wazazi kusikiliza redio Dodoma FM na redio za ndani ya jiji la Dodoma na kuwahimiza wanafunzi kusikiliza redio hizo ili kunufaika na vipindi vinavyoendelea na kufanya mazoezi kadiri yanavyotolewa na walimu wabobezi. Kuhusu ratiba amesema kuwa inapatikana katika tovuti a Jiji la Dodoma www.dodomacc.go.tz na kwa watendaji wa kata na mitaa, walimu na wakuu wa shule zote jijini Dodoma.

Ikumbukwe kuwa mkakati wa kuwanusuru wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wa jiji la Dodoma ulizunduliwa na Mkurungenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi tarehe 28 Aprili, 2020 katika ukumbi  wa mikutano wa Halmashari ya Jiji la Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.