• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali inaendelea kuchukua hatua ndoa na mimba za utotoni- Dkt. Dugange

Imewekwa tarehe: September 10th, 2022

Angela Msimbira, OR-TAMISEMI

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Dkt.Festo Dugange amesema serikali kwa kushirikiana na wadau wa elimu nchini inaendelea kuchukua hatua stahiki kuhakikisha vitendo vya unyanyasaji na ukatili dhidi ya watoto ikiwemo mimba na ndoa za utotoni zinatokomezwa nchini.

Ameyasema hayo leo tarehe 9 Septemba, 2022 jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwenye hafla fupi ya utoaji wa zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri kwenye insha iliyohusu mimba na ndoa za utotoni.

Amesema kuwa Serikali imeendeleza jitihada za kudhibiti ndoa na mimba za utotoni ambapo kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ambayo imekuwa ikitoa sera, Waraka na miongozo mbalimbali ili kukabiliana na changamoto hizo ambapo Ofisi ya Rais-TAMISEMI imeendelea kusimamia utekelezaji wake.

Dkt. Dugange ametaja miongozo na Waraka zilizotolewa ili kukabiliana na mimba na ndoa za utotoni kuwa ni Waraka wa Elimu Namba mbili wa mwaka 2008 na kuanzishwa kwa mwongozo wa Mwaka 2022 wa kurejesha shuleni wanafunzi waliokatiza masomo katika elimu ya msingi na sekondari.

Ameendelea kufafanua kuwa katika mwaka 2016 hadi 2022 Serikali imefanya mageuzi makubwa katika sekta ya elimu hususani katika bajeti ya elimu bila ada na ujenzi wa miundombinu ya shule lengo likiwa ni kuboresha elimu msingi na sekondari.

Aidha, amesema kuwa kuwalinda wanafunzi wasiingie kwenye changamoto mbalimbali serikali imeweza kuboresha miundombinu ya shule za msingi na sekondari kwa kujenga madarasa na mabweni.

Dkt. Dugange ametoa rai kwa viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kufanya jitihada za kuwatambua wadau wa elimu waliopo katika maeneo yao kuhakikisha wanawashirikisha katika kutatua changamoto zilizopo badala ya kusubiri kila changamoto itatuliwe na Serikali.

Naye, Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Bodi ya World Vision Tanzania, Dkt.Diana Mdeme ameiomba Serikali kuendelea kusimamia sheria na kuchukua hatua stahiki kwa wanaohusika katika kusababisha mimba na ndoa za utotoni.


Chanzo: Tamisemi

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.