• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali kuendelea kuzisaidia Serikali za Mitaa

Imewekwa tarehe: May 9th, 2019

OFISI ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa imesema itaendelea kutoa ushirikiano kwa mamlaka za Serikali za mitaa ili ziweze kutekeleza majukumu yake ya kuwaletea maendeleo Wananchi.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo katika hotuba yake wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba wa ushauri katika utafiti na usanifu wa mfumo wa utiririshaji wa maji ya mvua na maandalizi ya mpango wa uboreshaji wa mifumo ya mitaro ya maji ya mvua na maji taka katika jiji la Dodoma kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2020 hadi 2040.

“Ofisi ya Rais TAMISEMI itaendelea kutoa ushirikiano kwa mamlaka za Serikali za Mitaa ili ziweze kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria” alisema Jafo.

Akiongelea utekelezaji wa mkataba huo, alisema kuwa mshauri msanifu ni mtu muhimu sana katika ufanisi wa mradi na kuwa, anategemea kazi ya utafiti na usanifu katika mradi huo itafanyika vizuri ili kuondoa matatizo yanayozuilika wakati wa utekelezaji wa mradi huo.

“Tunataka wakati wa utekelezaji wa mradi huu ujibu shida za wananchi katika jiji la Dodoma, tunataka Jiji hili lipangwe vizuri na watu waje kutoka maeneo mengine kufanya utalii Dodoma” alisisitiza.

Aidha, Waziri Jafo alitoa pongezi kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kusimamia shughuli za Halmashauri hiyo kwa weledi mkubwa.

“Pongezi kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kufanya kazi nzuri, naomba Mungu asaidie ubaki hapa ili uendeleze mazuri yako” alisema.

Wakati huo huo, Waziri Jafo ameipongeza Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kufanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato. “Jiji la Dodoma ndiyo Jiji pekee linaloongoza kwa ukusanyaji wa pato ghafi kwa Halmashauri zote nchin...hongereni sana Jiji la Dodoma kwani mapato yenu  ya ndani yanaweza kuendesha Halmashauri nyingine bila serikali kuu kuongeza fedha, Hakika Dodoma ni Jiji la mfano hongereni sana” alisema Waziri Jafo.

Awali, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi alisema kuwa mradi wa ushauri katika utafiti na usanifu wa mfumo wa utiririshaji wa maji ya mvua na maandalizi ya mpango wa uboreshaji wa mifumo ya mitaro ya maji ya mvua na maji taka katika Jiji la Dodoma kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2020 hadi 2040 unalenga kukidhi mahitaji halisi ya Jiji pamoja na kutunza mandhari.

Kunambi alisema kuwa, usanifu wa mradi huo utatoa suluhisho la kudumu katika kupambana na mafuriko ya mara kwa mara katika Jiji la Dodoma ambapo utaweka mfumo thabiti wa ukusanyaji wa maji taka ili kuhakikisha mazingira ya jiji yanabaki kuwa nadhifu wakati wote.

Mradi huo utatekelezwa na mshauri msanifu kampuni ya Cheil Engineering Co. Ltd kutoka Jamhuri ya Korea Kusini kwa kushirikiana na kampuni ya AJOMA Consult Ltd. ya Tanzania kwa mkataba wenye gharama ya Shilingi 1,575,573,813.10, ambao utatekelezwa kwa muda wa miezi 12 kuanzia tarehe Mei 6, 2019 mpaka Mei 5, 2020.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.