• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali kujenga shule 1,026

Imewekwa tarehe: February 15th, 2021

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itajenga shule mpya 1,026 ambapo kati ya hizo, shule 26 zitakuwa za bweni zenye uwezo wa kupokea wanafunzi kati ya 1,000 hadi 1,500 kwa kila mkoa na zitajengwa kwa awamu tatu.

Ametoa kauli hiyo Jumamosi, Februari 13, 2021 katika hotuba yake aliyoitoa wakati wa kuahirisha mkutano wa pili wa Bunge jijini Dodoma. Bunge limeahirishwa hadi Machi 30, mwaka huu.

Waziri Mkuu amesema shule nyingine mpya 1,000 za kutwa zenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 400 kwa kila shule, zitajengwa chini ya mradi wa maboresho ya elimu ya sekondari yaani Secondary Education Quality Improvement Programme (SEQUIP) ambao utatekelezwa kwa muda wa miaka mitano (2020/2021 – 2025/2026).

Amesema Benki ya Dunia iliidhinisha mkopo wa kiasi cha dola za Marekani milioni 500 sawa na sh. trilioni 1.2 kwa ajili ya mradi huo, na kwamba ukikamilika, utakuwa ni mwarobaini kwa changamoto ya miundombinu ya shule za sekondari.

“Shule hizo zitajengwa kwenye kata 718 zisizo na sekondari za kata na kwenye maeneo yaliyoelemewa na idadi kubwa ya wanafunzi. Hivyo basi, nitumie nafasi hii kuwaelekeza viongozi na watendaji wa Serikali za Mitaa wasimamie kikamilifu utekelezaji wa mradi huu ili kufikia malengo yaliyokusudiwa,” amesisitiza.

Wakati huohuo, akielezea suala la ukuzaji ujuzi miongoni mwa vijana, Waziri Mkuu amesema katika kipindi cha Julai, 2020 hadi Januari, 2021 vijana 10,178 wamepatiwa mafunzo na kutathminiwa ujuzi walioupata nje ya mfumo rasmi wa mafunzo nchi nzima ambapo vijana 9,736 wamefaulu na kupatiwa vyeti na Mamlaka ya Mafunzo na Ufundi Stadi (VETA).

Amesema vyeti hivyo vinawawezesha vijana hao kutambulika, kujiendeleza kiujuzi, kujiajiri pamoja na kupata kazi katika taasisi na kampuni mbalimbali. “Vijana hao ni wenye ujuzi katika fani za uashi, useremala, ushonaji, ufundi bomba, uchomeleaji na uungaji vyuma, ufundi magari, ufundi umeme, ukarabati wa bodi za magari, upishi na uhudumu katika hoteli. Aidha, vijana 36 wamegharamiwa na Serikali kwa ajili ya kuhudhuria mafunzo ya kilimo cha kisasa nchini Israel,” amesema.

“Katika nusu ya pili ya mwaka 2020/2021, vijana wapatao 4,616 watapatiwa mafunzo na kurasimishwa ujuzi walionao kupitia mfumo huu. Aidha, Januari 2021, vijana 1,203 wa vyuo vya elimu ya juu na kati wamehitimu mafunzo ya uzoefu wa kazi kupitia kampuni mbalimbali kulingana na fani walizosomea, na wahitimu 2,037 wamewezeshwa na wanaendelea kupata mafunzo ya uzoefu wa kazi katika taasisi binafsi na za umma ambayo yatachukua muda wa kipindi cha mwaka mmoja.”

Amesema wahitimu 2,421 wanaandaliwa ili waanze mafunzo Machi, 2021 katika fani za ushonaji nguo, useremala, uashi, uchorongaji vipuri, ufundi magari, umeme, bomba, terazo, upishi, na utoaji huduma za mahoteli, utengenezaji wa simu, majokofu, viyoyozi, upakaji rangi, uandishi wa alama, utengenezaji wa umeme wa magari, utengenezaji wa nywele na utanashati, uchoraji, n.k.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameeleza mikakati ya Serikali ya kuimarisha kilimo cha umwagiliaji nchini ambapo amesema katika kipindi cha mwaka 2015 hadi 2020, Serikali imefanikiwa kujenga na kukarabati skimu za umwagiliaji 179 ambazo zimeongeza eneo la umwagiliaji kutoka hekta 461,000 mwaka 2015 hadi hekta 694,715 mwaka 2020 sawa na ongezeko la asilimia 50.7.

“Hii ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Kabambe wa Taifa wa Umwagiliaji wa mwaka 2018 yaani Revised National Irrigation Master Plan (RNIMP 2018) ambao umeainisha hekta milioni 29.4 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji,” amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amesema Serikali imekamilisha ujenzi wa maghala 14 ya kuhifadhia mavuno katika skimu za umwagiliaji za Ngana na Makwale (Kyela), Magozi na Tungamalenga (Iringa), Mbuyuni-Kimani, Ipatagwa, Kongolo-Mswiswi na Motombaya (Mbarali), Lekitatu (Arusha), Mombo (Tanga), Uturo (Mbeya), Bagamoyo (Pwani), Mkindo na Mkula (Morogoro).

“Katika hatua ya kuongeza mnyororo wa thamani kwenye uzalishaji wa mazao ya kilimo, kati ya maghala hayo, maghala sita yamewekewa na vinu vya kukobolea mpunga,” ameongeza.


Kwa msaada wa Fullshangwe Blog

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.