• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali kujenga vituo vya uhifadhi matunda, mboga mboga

Imewekwa tarehe: November 28th, 2022

SERIKALI kupitia Wizara ya Kilimo inakamilisha taratibu za ujenzi wa Vituo vitatu vya ukusanyaji, uhifadhi na utengaji wa madaraja kwa lengo la kuwezesha ufanisi na ubora katika  usafirishaji wa mazao ya mboga mboga na matunda kutoka mashambani mpaka kumfikia mlaji wa mwisho ndani na nje ya nchi. Vituo hivyo vitajengwa katika bandari ya Dar es Salaam, Siha mkoani Kilimanjaro na Mufindi Mkoani Iringa.

Hayo yamesemwa leo tarehe 28 Novemba, 2022 na Naibu Waziri wa Kilimo, Mh. Anthony Mavunde alipokuwa akifungua Kongamano la Kimataifa la uthibiti ubora na viwango vya mazao ya mbogamboga na matunda lililofanyika  Jijini Arusha.

"Hatuwezi kufikia ubora wa masoko ya kimataifa ya mazao yetu ya mboga mboga na matunda nchini pasipo kujenga miundombinu wezeshi.

Serikali kupitia Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, imetoa fedha kwa ajili ya kuwezesha ujenzi wa Vituo vitatu vya ukusanyaji na uhifadhi wa mazao (common use facility) hayo ili yaweze kusafirishwa kwa ubora na viwango vya kimataifa.

Lengo ni kutoa kipaumbele kwa mazao ya mboga mboga na matunda kuanzia yanaposafirishwa kutoka mashambani mikoani mpaka yanaposafirishwa bandarini, mipakani ama kwenye viwanja vyetu vya ndege. Ni dhahiri kwamba mazao ya mboga mboga na matunda hayawezi kusafirishwa kwa kipaumbele sawa na bidhaa kama madini ya shaba au makaa ya mawe, lazima tuyape kipaumbele ili kutoharibu ubora wake.

Serikali imepanga kuongeza mapato kutokana na mauzo ya bidhaa za matunda na mboga mboga  nje ya nchi kutoka Dola za Kimarekani milioni 750 hadi bilioni 2 ifikapo Mwaka 2030. Ni matarajio yetu kwamba kama Nchi, tunashirikiana kwa pamoja Serikali nanyi wadau wote, kuweka mifumo thabiti ya ubora wa mazao yetu tunayouza nje ya nchi” Alisema Mavunde.

Awali, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi Kilele ya Wadau wa Mazao ya Horticulture (TAHA), Dkt. Jacqueline Mkindi alieleza lengo la kongamano hilo ni kutathmini mbinu bora za kilimo, kuangalia nafasi ya Nchi yetu ya Tanzania katika ushindani wa masoko ya Kimataifa, kuongeza wigo wa upatikanaji wa masoko ya uhakika na kuendelea kuelimishana juu ya uthibiti wa viwango vya ubora wa mazao yetu yanayouzwa nje ili kuongeza pato la mkulima na Taifa kwa ujumla.

Wakati huohuo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya TAHA, Mhandisi Zebadiah Moshi alishukuru ushirikiano wa dhati wa Serikali na kuongeza kuwa, baada ya mkutano huo wakulima wanaenda kuongeza uelewa wa namna ya kufikia viwango vya kimataifa na hivyo kuongeza mauzo ya nje.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa John Mongella alishukuru kwa mkutano huo kufanyika Mkoani Arusha, na kusisitiza kuwa milango ya Serikali ya Mkoa wa Arusha ipo wazi kwa TAHA na wadau wote kwenye mnyororo wa thamani wa mazao ya mboga mboga na matunda hivyo wakaribie watapata ushirikiano mkubwa katika jitihada za kuinua maisha ya wananchi na pato la Taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.