• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Shilingi Bilioni 125.69 kuimarisha huduma za afya ngazi ya msingi nchini

Imewekwa tarehe: September 3rd, 2020

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo wanaochangia sekta ya afya kupitia Mfuko wa Afya wa Pamoja (Health Basket Fund) imeridhia kuweka saini Hati ya Shilingi Bilioni 125.69 kwa ajili ya kuimarisha huduma za afya katika ngazi ya msingi nchini

Akiongea wakati wa kuidhinisha makubaliano hayo, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Mabula Mchembe amesema kuwa lengo kuu la Mfuko huo tangu kuanzishwa kwake mwaka 1999 ni Kuimarisha huduma za afya katika ngazi ya msingi (Halmashauri) zote nchini.

Amesema katika utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2020/21 Wadau nane (8) watachangia jumla ya USD 53.84 sawa na Shilingi bilioni 125.69 kwa kipaumbele cha kuimarisha huduma za afya katika vituo vya afya kwenye halmashauri zote 184 nchini.

“Shilingi bilioni 105.32 zitatumika kwa ajili ya kuimarisha utoaji wa huduma za afya katika vituo vya afya vipatavyo 5,533 kwenye halmashauri zote 184 nchini ikiwa ni pamoja na ununuzi wa dawa, vifaa na vifaa tiba, uendeshaji wa vituo, ukarabati mdogo na huduma za chanjo na vikoba. “Fedha hizo zitapelekwa moja kwa moja vituoni kwa utaratibu wa ‘Direct Health Facility financing” Alisema Prof. Mchembe.

Aidha, Prof' Mchembe alisema Shilingi bilioni 4.29 zitatumika kwa ajili ya kuziwezesha Timu za Afya za Mikoa 26 kufanya ufuatiliaji na usimamizi shirikishi katika halmashauri zote nchini na Shilingi bilioni 2.09 zitawezesha Ofisi ya Rais– TAMISEMI kusimamia na kutoa msaada wa kitalaam katika halmashauri na mikoa yote nchini.

Aliongeza kuwa Shilingi bilioni 5.13 zitawezesha Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kutekeleza masuala ya sera, mikakati na miongozo kwa ajili ya kuhakikisha huduma za afya zinatolewa kwa kiwango na ubora stahiki na Shilingi bilioni 8.86 zitakuwa kwa ajili ya kutekeleza maeneo mengine ya kipaumbele katika sekta.

“Vipaumbele tulivyoidhinisha na kamati ni pamoja na kutoa mafunzo kwa wataalam 620 wa dawa za usingizi; kununua machine za kisasa za kutolea dawa za usingizi katika vituo vya afya ngazi ya halmashauri na kufanya ukarabati mkubwa katika vyuo vinne (4) vya kutolea mafunzo ya watalaam wa afya”.

Prof. Mchembe alitaja maeneo mengine ya kipaumbele yaliyoidhinishwa na Kamati Kuu ya Mfuko huo kuwa ni kuhuisha Mkataba wa Makubaliano (MoU) baina ya pande zote mbili kwa kipindi cha 2021 – 2026, kununua mashine za kutolea dawa za usingizi katika vituo vya kutolea huduma za afya pamoja na kuvijengea uwezo vituo vya afya katika kusimamia na kutumia fedha kwa kuzingatia miongozo na taratibu mbalimbali.

Maazimio ya uwekaji saini Hati hiyo yamefanyika kwenye ofisi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto iliyoko mji wa Serikali Mtumba ambapo yalihudhuriwa na watalaam kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Wizara ya Fedha na Mipango, OR–TAMISEMI, Bohari ya Dawa na Wadau wa Maendeleo wanaochangia Mfuko huo kutoka Canada, Denmark, KOICA, Ireland, Switzerland, UNICEF, UNFPA na Benki ya Dunia. walioshiriki kwa njia ya ‘video conference’.


Chanzo: issamichuzi.blogspot.com


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.