• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali kutumia Trilioni 2.78 kutekeleza miradi ya elimu nchini

Imewekwa tarehe: September 26th, 2022

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Innocent Bashungwa amesema Serikali itatumia kiasi cha shilingi trioni 2. 78 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya elimu nchini.

Ameyasema hayo juzi tarehe 24 Septemba, 2022 jijini Arusha wakati akitoa taarifa  kwa umma kuhusu utekelezaji  wa miradi ya elimu nchini.

Mhe Bashungwa alisema kupitia mradi wa kuboresha Elimu ya Sekondari (SEQUIP) Serikali imetoa  Shilingi Trilioni 1.2 kwa lengo la kuongeza fursa za upatikanaji wa elimu ya Sekondari, kuweka mazingira salama kwa wasichana waliopo katika shule za Sekondari, na kuhakikisha wanafunzi wote wanamaliza elimu ya Sekondari na kufikia malengo yao.

Bashungwa alifafanua  kuwa Mradi wa Kuboresha Elimu ya Awali na Msingi (BOOST): Utatoa Shilingi Shilingi Trilioni 1.15. ambapo  utaboresha mazingira ya kujifunzia katika shule za umma kwa kujenga miundombinu ya elimu, kuimarisha umahiri wa walimu na ubora wa ufundishaji darasani, kwa kutoa mafunzo endelevu ya walimu kazini.

Programu ya Kutekeleza Elimu kwa Matokeo awamu ya Pili (EP4R II) itatoa Shilingi bilioni 435.90 kwa lengo la kuendelea kujenga miundombinu mbalimbali ya shule yaani madarasa, vyoo, mabweni na nyumba za walimu, pamoja na kununua vifaa vya kufundishia.

Alieleza kuwa afua zitakazotekelezwa ni pamoja Ujenzi wa Vyumba vya madarasa, Ujenzi wa Nyumba za Walimu, Ujenzi wa Maktaba, Ujenzi wa Matundu ya Vyoo, Ujenzi wa Mabweni, Ujenzi wa Mabwalo, Ujenzi wa Maabara, Ujenzi wa vyumba vya TEHAMA, Kutoa mafunzo endelevu kwa walimu kazini, na Ununuzi wa Vifaa vya TEHAMA.

Aidha Waziri Bashungwa amewaagiza Wakuu wa Mikoa wote nchini kuhakikisha wanafuatilia miradi yote ya Maendeleo ambayo fedha zake zipo kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa na inakamilishwa iifikapo tarehe 31 Oktoba, 2022 na wakurugenzi watakaoshindwa kukamilisha miradi ya Maendeleo ifikapo tarehe hiyo taarifa itolewe ili hatua stahiki zichukuliwe dhidi yao.

Pia amewataka wakuu hao wa Mikoa kuhakikisha wanawasimamia Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa ufanya matumizi sahihi ya fedha zote za miradi kwa kufuata Miongozo inayotolewa juu ya fedha hizo ili kupata thamani halisi ya fedha hizo kwa miradi inayotekelezwa.

Bashungwa ameelekeza kuhakikisha ufuatiliaji wa karibu wa ujenzi wa miundombinu ya miradi ya maendeleo wanayoletewa ili kuepuka hoja za ukaguzi zisizo za lazima.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.