• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali kutunga Sheria kulinda maeneo yanayofaa kwa kilimo - Mavunde

Imewekwa tarehe: October 17th, 2022

NAIBU Waziri wa Kilimo Mhe. Anthony Mavunde amesema serikali ipo njiani kutunga sheria maalum kwa ajili ya kilimo ili kulinda maeneo yote yanayofaa kwa kilimo katika azma yake ya kukuza sekta ya kilimo nchini.

Mheshimiwa Mavunde ameyasema hayo jana wakati akizungumza na wananchi wa kata ya Ihusi - Bariadi, Mkoani Simiyu katika mkutano wa hadhara wakati kamati ya mawaziri 8 wa kisekta wanaoshughulikia migogoro ya ardhi ya Vijiji 975 walipofika katika eneo hilo.

“Katika kulinda maeneo yanayofaa kwa kilimo na kupunguza migogoro ya matumizi ya ardhi nchini, serikali kupitia wizara ya kilimo tunaendelea na hatua za utungwaji wa sheria ya kilimo.

Kwakuwa dhamira yetu kubwa ni kuhakikisha tunakuza sekta hii ya kilimo kwa asilimia 10 ifikapo mwaka 2030, hatua hii lazima iende sambamba na kuyatambua maeneo ya kilimo na kuyalinda kisheria.

Katika maeneo yote ya utatuzi wa migogoro hii ambapo ardhi inamegwa kwa ajili ya kuwagawia wananchi kuendelea na shughuli za uzalishaji mali, mamlaka za upangaji wa matumizi bora ya ardhi katika maeneo husika hakikisheni mnatenga maeneo ya mashamba makubwa ya pamoja ya kilimo (block farms) ili serikali iweze kuwahudumia wakulima kwa urahisi” Alisema Mavunde.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Mavunde ametoa rai kwa wakulima wote kuendelea na kukamilisha zoezi la usajili wao ili wanufaike na huduma mbalimbali kutoka serikalini na hasa mbolea ya ruzuku ambapo serikali imetenga zaidi ya Tsh 150 bilioni kama sehemu ya ruzuku ya mbolea ili kumpunguzia mzigo mkulima.

Hatua hiyo inafuatia kupanda kwa bei ya mbolea katika soko la dunia jambo linalowafanya wakulima wa kawaida kushindwa kumudu kununua mbolea na hivyo kuathiri kukua kwa uzalishaji wa mazao ya kilimo nchini.

Amesema kiasi hicho cha fedha kilichotengwa kitawawezesha wakulima kununua mbolea kwa nusu bei iliyopo kwenye soko.

NAIBU Waziri Mavunde alitumia wasaa huo pia kumshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza bajeti ya  Wizara ya Kilimo kutoka Bilioni 294 hadi Bilioni 954 ambapo Shilingi Bilioni 400 zimeelekezwa katika kilimo cha umwagiliaji hasa katika kuyafanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina mabonde yote makubwa nchini sambamba na ujenzi wa mabwawa mapya 13.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.