• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali ya awamu ya sita inatekeleza miradi mingi ya maendeleo- Diwani Sanga

Imewekwa tarehe: June 16th, 2023

Na. Theresia Nkwanga, TAMBUKARELI

SERIKALI ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan inatekeleza miradi mingi ya maendeleo kwa lengo la kuwaletea maendeleo wananchi wa Kata ya Tambukareli.

Kauli hiyo ilitolewa na Diwani wa Viti Maalum Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Leticia Sanga alipokuwa akiongea na wananchi wa kata ya Tambukareli katika ziara ya madiwani wa viti maalum wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuwahamasisha wananchi waliokopa kurejesha mikopo ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Sanga alisema kuwa serikali ya Awamu ya Sita imepeleka fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo Dodoma na hasa katika kata ya Tambukareli. “Wananchi wote tunaona mama yetu Samia Suluhu Hassan anavyojenga shule, zahanati na barabara. Nafikiri mnaona kila mahali kuna shule nzuri na barabara nzuri, Anajenga zahanati na hospitali nzuri ili tukiugua tukahudumiwe vizuri, tukitaka kujifungua tujifungue salama. Vilevile, nimpongeze sana Rais kwa kuzindua Ikulu hapa Dodoma, maana yake makao makuu ya Tanzania ni rasmi Dodoma” alisema Sanga.

Aidha, alimshukuru kwa utekelezaji miradi ya kitaifa. “Tunamshukuru mama Samia kuendeleza miradi yote iliyoanzishwa na mwenda zake Rais, Dkt. John Magufuli mfano miradi ya barabara ya mzunguko Dodoma, Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Msalato unaendelea. Miradi mipya ambayo ameibuni mama inasimamiwa vizuri na inaendelea. Kipekee nimshukuru kaka yangu Joseph Mafuru, Mkurugenzi wetu wa Jiji la Dodoma kwa kazi nzuri anayoifanya kwa kusimamia fedha zote za miradi anazopewa na Mheshimiwa Rais ili Dodoma Jiji iweze kuwa imara na kupendeza zaidi” alisema Sanga.

Akiongelea mikopo inayotolewa na Halmashauri ya jiji kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu alisema inalenga kuwakomboa wananchi kiuchumi. “Halmashauri ya Jiji la Dodoma inatoa mikopo ya asilimia 10 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Mikopo hii haina riba. Ni fursa kwa wananchi wetu kujikomboa kiuchumi kwa kukuza mitaji yao. Nitumie nafasi hii kuwahimiza wakopaji wote kuhakikisha mnarejesha mikopo hiyo ili iweze kunufaisha watu wengi zaidi” alisema Sanga.

Aidha, alimpongeza Diwani wa Kata ya Tambukareli, Juma Michael kwa kazi nzuri na usimamizi wa shughuli za maendeleo katika kata hiyo. “Mheshimiwa Diwani anaisemea vizuri kata hii, hivyo muendelee kumuunga mkono. Kipekee nimshukuru Mbunge wa Jimbo la Dodoma mjini kwa kazi nzuri za maendeleo anazofanya hapa Dodoma kuhakikisha miradi yote ya maendeleo inaenda vizuri” alisema Sanga.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.