• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali ya awamu ya sita yasogeza huduma ya afya kwa wananchi

Imewekwa tarehe: April 19th, 2024

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeshuhudia ongezeko kubwa la ujenzi wa vituo vya afya nane katika serikali ya awamu ya sita inayolenga kuongeza miundombinu na kusogeza huduma za afya karibu na wananchi.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Divisheni ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Andrew Method alipokuwa akiongelea mafanikio ya miaka mitatu ya serikali ya awamu ya sita kwa waandishi wa habari ofisini kwake jijini hapa.

“Ndugu waandishi wa habari, katika kipindi hiki cha miaka mitatu ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita tumeshuhudia ongezeko kubwa la ujenzi wa vituo vya afya katika Jiji la Dodoma, tumejenga vituo vya afya nane. Mpaka sasa vituo viwili vimekamilika. Kituo cha Afya Chang’ombe kimekamilika. Mnafahamu eneo la Chang’ombe lina wakazi wengi zaidi ya 40,000 lakini hawakuwa na kituo cha afya. Pia tumekamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Nkuhungu. Kama mnavyofahamu mnaokuja Dodoma, eneo lote la Nkuhungu halikuwa na huduma za afya, lakini serikali ya awamu ya sita katika kipindi cha miaka mitatu mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha tukaanza ujenzi na kukamilisha Kituo cha Afya Nkuhungu” alisema Dkt. Method.

Aliongeza kuwa eneo la Nzuguni vinajengwa vituo vya afya viwili. “Kituo kimoja kinajengwa Ilazo, barabara ya Marthin Luther na kipo hatua za mwisho za umaliziaji. Kituo tayari vifaa tiba vimeshafika na mafunzo kwa watumishi yametolewa na tunategemea mwezi wa Julai, 2024 kianze kufanya kazi. Ni mradi mkubwa ambao umegharimu takribani shilingi bilioni 2.8 kwa hiyo unaweza kuona kwa kiasi gani Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi hizo kwa kuwezesha huduma za afya ziwe bora katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma” alisema Dkt. Method.

Dkt. Method ambae pia ni Mganga Mkuu wa Jiji la Dodoma alisema kuwa serikali inajenga vituo vya afya vinne katika barabara ya mzunguko ‘ring road’. “Ukiangalia kwenye uboreshaji wa miundombinu, mheshimiwa Rais anajenga barabara lakini pia anajenga na vituo vya afya ambavyo vitatoa huduma kwenye hiyo barabara ya mzunguko. Vituo hivyo vitajengwa katika Kata ya Ihumwa, Kata ya Nzuguni eneo la Mahomanyika, Kata ya Nala na Kata ya Makutopora. Kwa hiyo, utaona ni uwekezaji mkubwa sana wa hivi vituo ambavyo vinajengwa. Kwa ujenzi tu wa hivi vituo, kuna wananchi zaidi ya 400,000 wanawenda kunufaika kwa sababu hivi vituo vinajengwa katika maeneo ambayo yanawakazi zaidi ya 50,000 kwenye kata” alisema Dkt. Method.

Akiongelea ujenzi unaoendelea wa vituo viwili vya afya vya Kizota na Zuzu alisema vipo hatua za mwisho kukamilika. “Halmashauri ilipeleka fedha kwa maelekezo ya mheshimiwa Rais kujenga kituo cha Afya Kizota ili kihudumie wananchi wa Kata ya Kizota. Kituo kipo katika hatua za mwisho kukamilika. Pia kuna ujenzi wa kituo cha afya katika Kata ya Zuzu, nacho kipo katika hatua za mwisho kabisa kukamilika. Ukiangalia miundombinu hii ambayo inajengwa, utaona ni jinsi gani mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alivyodhamiria kuliweka Jiji la Dodoma katika mpango mkakati wa kuweza kupokea ongezeko la watu kama makao makuu” alisema Dkt. Method.





Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.