• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Serikali yakabidhi Hosteli ya Furaha kwa Chuo cha Mipango Dodoma

Imewekwa tarehe: September 18th, 2019

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, TAMISEMI Mhandisi Joseph Nyamhanga amekabidhi majengo na eneo lililokuwa linamilikiwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini - IRDP.

Akiongea katika hafla fupi ya makabidhiano ya majengo na eneo hilo lililopo katikati ya Jiji la Dodoma barabara iendayo Iringa, Mhandisi Nyamhanga amesema awali majengo hayo yalikuwa yakimilikiwa na iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA) na baada ya kuvunjwa kwake yalikabidhiwa kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Chuo cha Mipango walikuwa wapangaji katika majengo hayo.

“Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini kilikuwa kinapanga hapa na kilikuwa kinalipa gharama kubwa, naambiwa zaidi ya shilingi milioni 250 kwa mwaka kwa ajili ya wanafunzi kusoma, lakini sasa Serikali imeamua kwamba hosteli hii ikabidhiwe kwa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini kilichopo Jijini Dodoma”.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo kwa kubadilishana hati kati ya Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhandisi Joseph Nyamhanga kwa niaba ya Serikali na Mkuu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo ya Vijijini Profesa Hozen Mayaya.

Mhandisi Nyamhanga amemtaka Mkuu wa Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini kukarabati majengo hayo lakini pia kuondoa majengo ya muda yaliyokuwa yakitumiwa kama madarasa na kujenga majengo mapya ya kudumu kwa kuwa sasa hawapangi tena na wao ndio wamiliki.

Amewataka wanafunzi wote wa chuo hicho kusoma kwa bidii na kuinua kiwango cha ufaulu. Nyamhanga amemshukuru Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambaye amekuwa mstari mbele na kufanya jitihada kubwa za kuboresha elimu kuanzia shule za awali, msingi, sekondari, vyuo vya ufundi na vyuo vikuu nchini.

Kwa upande wake Mkuu wa chuo cha Mipango Profesa Hozen Mayaya ameishukuru Serikali kwa maamuzi mazuri ya kuwakabidhi majengo hayo na eneo ambalo litasaidia kuboresha miundombinu na mazingira rafiki ya kujifunzia kwani gharama za upangaji katika majengo hayo zilikuwa kubwa ambazo ni zaidi ya milioni 252 kwa mwaka.

Aidha, Mayaya alisema Chuo cha Mipango bado kina uhitaji wa miundombinu ya majengo ya madarasa na hosteli kutokana na kudahili wanafunzi wengi kutoka mikoa karibu yote hapa nchini.

Katika makabidhiano hayo Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma aliwakilishwa na Elihuruma Mufuruki, Mkuu wa Kitengo cha Manunuzi wa Jiji la Dodoma.

Chanzo: Tovuti ya tamisemi.go.tz


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.